Wednesday, October 31, 2012

WANAHABARI NCHINI WATAKIWA KUANDIKA NA KUTOA MAONI KUHUSIANA NA MCHAKATO WA KUPATA KATIBA MPYA

 Deus Kibamba -Mwenyekiti wa jukwaa la Katiba
Na Joseph Mwambije,
Dodoma
WAANDISHI wa habari Nchini wametakiwa kuandika  na kutoa maoni yao kuhusiana na mchakato wa kupata Katiba mpya ili Wananchi wajue kinachoendelea na kwamba umakini unatakiwa ili iweze kupatikana Katiba bora.
Wito huo umetolewa  jana(leo) na Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Bw. Deus Kibamba wakati akitoa mada kuhusiana na Mchakato wa kupata Katiba mpya kwa Waandishi wa habari zaidi ya 36 kutoka Mikoa mbalimbali Nchini ambao wanapatiwa mafunzo ya siku mbili ya kujengewa uwezo wa wa kuandika habari kuhusiana na mchakato  wa Katiba mpya.
‘Waandishi pelekeni maoni yenu kuhusiana na mchakato wa kupata katiba mpya na pia muandike habari na makala kuhusiana na Katiba mpya ili tupate Katiba bora yenye maslahi kwa Taifa na wananchi’anasema Bw. Kibamba.
Alisema kuwa Watanzania wasipokuwa  amakini itapatikana Katiba mbovu kuliko iliyopo sasa hivyo alisisitiza kuwa umakini unatakiwa katika kuelekea kupatikana kwa Katiba mpya.
Mwenyekiti huyo wa jukwaa la Katiba alisema kuwa Sauti ya Jukwaa la Katiba itapelekwa kwa wananchi na Wanahabari na kwamba Jukwa hilo pia linalinda Katiba iliyopo isivunjwe na ndio  maana alisema kuwa alipouawa Marehemu Daud Mwangosi wa  hawakunyamaza kwa kuwa Katiba  ilivunjwa.
Alisema kuwa katika mchakato wa kupata Katiba mpya Wanahabari wana nafasi  ya pekee na kuwahamasisha waandishi wa habari kuandika habari kuhusiana na Mchakato wa kupata Katiba mpya uanaoendelea.
Aliwataka Wanahabari kutokuwa waoga kuandika habari  za Katiba na kubainisha kuwa wale watakaonyanyaswa kwa kuandika habari za mchakato wa Katiba mpya Sheria itawalinda.

 Wanahabari wakifuatilia kwa makini mada katika Ukumbi wa Dodoma Hotel Mjini Dodoma.
 Bw. Abdinery Chihimba Mtoa mada kutoka Kenya akitoa uzoefu wa Nchi hiyo kupata Katiba mpya
 Watoa mada Profesa Abdul Sharif  wa Baraza  la Katiba Zanzibar na Deus Kibamba wakisikiliza kwa makini uzoefu wa Katiba mpya ya Kenya.

 Mmoja wa washiriki Bw. Kimambo kutoka Kilimanjaro akifuatilia kwa makini.

No comments:

Post a Comment