Monday, September 17, 2012

Wauwaji wa balozi wakamatwa Libya

Wauwaji wa balozi wakamatwa Libya

Na Mashirika ya habari
Libya
Mkuu wa bunge la Libya anasema kuwa watu kama 50 wamekamatwa kwa kuhusika na mauaji ya balozi wa Marekani mjini Benghazi juma lilopita.
MegaryefKiongozi wa Bonge Bw. Megaryef.

Mohammed Megaryef, kiongozi wa bunge, alisema hakuna shaka kuwa shambulio hilo lilikuwa limepangwa na siyo tu la kulipiza kisasi kwa filamu ya Marekani iliyokejeli Uislamu.
Akizungumza na shirika la habari la Canada, CBS, Bwana Megaryef alisema anaamini wageni wenye uhusiano na Al-Qaeda walihusika.
Balozi wa Marekani, Chris Stevens, na Wamarekani wengine watatu, waliuwawa wakati guruneti lilipopiga ubalozi mdogo wa Marekani mjini Benghazi na kuwaka moto.

No comments:

Post a Comment