Thursday, August 30, 2012

Polisi watatu wafariki kufuatia ghasia Mombasa

 Na Mashirika ya habari,
Kenya
Fujo zaendelea Mombasa kwa siku ya pili mfululizo.

Hali ya wasiwasi ingali imetanda mjini Mombasa kwa siku ya tatu baada ya ghasia za siku mbili kufuatia kifo cha mhubiri wa kiisilamu Sheikh Aboud Rogo siku ya Jumatatu.
Inaarifiwa vijana wanalenga kufanya mashambulizi ya kuvizia wakirusha matairi na vifaa vingine barabarani na kisha kutoroka, licha ya kuwa polisi wanashika doria.
Polisi wawili wamethibitishwa kufariki kutokana na majeraha yao baada ya shambulio la guruneti dhidi ya gari lao mjini Mombasa hapo jana.
Hadi kufikia sasa polisi watatu wamefariki tangu kuanza kwa ghasia zilizotokea baada ya kifo cha mhubri wa kiisilamu mwenye siasa kali Sheikh Aboud Rogo siku ya Jumatatu.
Kwa siku mbili, vijana wa kiisilamu wamekuwa wakipambana na polisi katika barabara za Mombasa wakifanya uharibifu kuchoma magari na kupora maduka pamoja na kuvamia makanisa mjini humo. Watu wengine kumi na tatu walijeruhiwa vibaya katika shambulio hilo.
Mhubiri Aboud Rogo Mohammed, alikuwa mshukiwa wa ugaidi na pia alishukiwa kufadhili kundi la wanamgambo la Al Shabaab nchini Somalia.
Wakati huohuo, watu 12 wamekamatwa na polisi kufuatia makabiliano kati ya polisi na vijana wanaofanya vurugu kufuatia kuuwawa kwa kiongozi wa kidini Sheikh Aboud Rogo siku ya jumatatu.
Katika siku ya pili ya vurugu hizo, wengi ya vijana hao wamekamatwa nje ya Msikiti Musa iliyo eneo la Majengo visiwani Mombasa.
Wakati wa makabiliano hayo polisi walitumia gesi ya kuolisitoa machozi kuwatawanya waandamanaji waliokuwa na ghadhabu.
Hata hivyo katika eneo moja polisi walilazimika kutumia risasi za mpira kuwatawanya vijana waliokuwa wakiwasha matairi barabarini na kufanya uporaji.
Bwana mmoja alichomwa kisu katika karakana yake na kulazimika kupewa huduma ya kwanza na wafuasi wa dhehebu la Jeshi la wokovu.
Na wakati Mombasa ikiwaka moto, wapiganaji wa Al shabaab wametuma ujumbe katika mtandao wao wakiwasihi waislamu wa Kenya "wachukuwe kila hatua zinazostahili kulinda dini yao"
" Waislamu lazima wachukue sheria mikononi mwao, na wasimame kidete dhidi ya makafiri na kuchukua kila hatua kuilinda dini yao, heshima yao ,mali yao na maisha yao kutoka kwa maadui wa waislamu" , Al shabaab wamenukuliwa wakisema hayo katika taarifa yao.
Kiongozi huyo wa kidini Sheikh Aboud Rogo ,aliyepigwa risasi na kuuwa siku ya jumatatu alikuwa ametajwa na Marekani pamoja na Umoja wa Mataifa kama mtua anayewasajili baadhi ya vijana wa Kenya wkenda kujiunga na wapiganaji wa Al Shabaab.
Sheikh Aboud Rogo pia anadaiwa kuwa alikuwa mfadhili wa kundi hilo la Al shabaab.

Operesheni kali dhidi ya wapigananaji Sinai



 
Na Mashirika ya habari
Ulinzi mkali Sinai
Maafisa wa usalama nchini Misri, wamewaua wapiganaji kumi na moja tangu kuanzisha operesheni kali dhidi ya wapiganaji hao katika rasi ya Sinai, mapema mwezi huu . Hii ni kwa mujibu wa taarifa za wizara ya ulinzi nchini Misri.
Operesheni hiyo, iliyoanzishwa baada ya kuuawa kwa walinzi kumi na sita wa mpakani katika shambulizi lililofanywa tarehe tano mwezi huu, pia imewezesha kukamatwa kwa washukiwa 23 na hata kunasa silaha.
Maafisa wengine wa ulinzi walitarajiwa kepelekwa huko hii mnamo Jumatano kuweza kukamilisha msako wa washukiwa wa ugaidi.
Hata hivyo, hatua ya kuongeza idadi ya wanajeshi mpakani tayari imeweza kuzua wasiwasi kwa serikali ya Israel.
Tangu mwaka 1982, wakati wanajeshi wa Israel walipoondoka mpakani eneo la sinai limesalia chini ya ulinzi mkali, kufuatia makubaliano ya amani kati ya nchi hizo mbili ambayo yalisainiwa mwaka 1979, ambayo yanazuia Misri kutumia nguvu za kijeshi katika eneo hilo.
Mnamo siku ya Jumatatu,rais wa Misri, Mohammed Mursi alisisitiza kuwa nchi yake itatii mikataba yote ya kimataifa na bila ya kutaja Israel ikasema kuwa hakuna nchi zingine zinapaswa kuwa na wasiwasi kuhusu hatua zake huko Sinai.
Misri ilianzisha operesheni yake ya usalama kwa jina "Operation Eagle", ambayo imehusisha maelfu ya wanajeshi wakisaidiwa na vifaru na silaha zingine nzito baada ya walinzi kumi na sita kuuawa katika operesheni dhidi ya kambi yao karibu na ukanda wa Gaza.
Baada ya kuwaua wanajeshi, wapiganaji hao walivuka mpaka na Israel katika jariibio lao kufanya shambulizi lengine. Ingawa waliuawa katiakmashambulizi ya angani yaliyofanywa na Israel.
Hata hivyo yeyote amewajibika na mashambulizi hayo ingawa wanaoshukiwa sana kuhusika ni makundi ya wapiganaji ambayo yanajulikana kwa kuendesha shughuli zao mashariki mwa Sinai.
Katika siku za kwanza za operesheni hiyo majeshi yalifanya msako mkali katika maficho ya wapiganaji hao.

Monday, August 27, 2012

CCM yawatosa vigogo watuhumiwa wa ufisadi

 
Monday, 27 August 2012 07

*KAMATI KUU YATOA TAMKO KUWAPONGEZA MAWAZIRI WALIOWAWAJIBISHA WATENDAJI WA MASHIRIKA YA UMMA
Raymond Kaminyoge
KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (CC), imewapongeza mawaziri kwa kuchukua hatua dhidi ya watendaji wanaotuhumiwa kwa vitendo vya matumizi mabaya ya ofisi za umma wakiwamo wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na kuwataka waendelee na kasi hiyohiyo.
Pongezi hizo za Kamati Kuu zimetolewa baada ya kikao chake kilichofanyika Ijumaa iliyopita na zimekuja baada mawaziri kadhaa kuwachukulia hatua za kinidhamu baadhi ya watendaji walio chini ya wizara zao kwa tuhuma mbalimbali.
Mawaziri waliowachukulia hatua watendaji ni pamoja na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda.
Juzi, Kamati Kuu iliipongeza Serikali kwa kutekeleza maagizo yake ya kutaka ichukue hatua dhidi ya watendaji waliohusishwa katika ubadhilifu katika mashirika ya umma.
“Kamati Kuu inawapongeza mawaziri walioanza kutekeleza maagizo hayo kwani mwisho wa siku maisha bora kwa kila Mtanzania yatawezekana,” ilisema taarifa iliyotolewa jana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.
Kamati Kuu ilieleza katika taarifa yake kuwa ipo haja ya kuwachukulia hatua watendaji wakuu wa mashirika yaliyohusishwa na ubadhirifu mbalimbali na kwamba kitendo hicho cha mawaziri hao ni kutekeleza agizo lake.
Mei 17, mwaka huu, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Kigoda alimsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Charles Ekelege ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zikimkabili.
Miongoni mwa tuhuma hizo ni pamoja na kuyapa zabuni kampuni hewa za ukaguzi wa magari kabla hayajaingia nchini.
Muda mfupi baadaye, Juni 5, mwaka huu, Dk Mwakyembe alimsimamisha kazi Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Paul Chizi kutokana na tuhuma mbalimbali.
Hivi karibuni, pia Dk Mwakyembe alisimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraim Mgawe, wasaidizi wake wawili na Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam, Cassian Ng'amilo kupisha uchunguzi wa wizi wa vitu mbalimbali yakiwemo makontena 40 ya vitenge katika Bandari ya Dar es Salaam.
Pia aliwasimamisha kazi Meneja wa Kituo cha Mafuta ya Ndege Kurasini (Kurasini Oil Jet - KOJ), Meneja wa Kituo cha Mafuta JET na mhandisi wa mafuta wa kituo hicho, baada ya kubainika kuwepo kwa wizi wa mafuta.
Waziri Kagasheki kwa upande wake, alimfukuza kazi Mkurugenzi wa Wanyamapori, Obeid Mbanga kwa kashfa ya kusafirisha wanyama kwenda nje ya nchi.
Julai 14, mwaka huu, Bodi ya Tanesco ilimsimamisha kazi  Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, William Mhando ikielezwa kuwa ni maelekezo ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Muhongo ili kupisha uchunguzi wa matumizi mabaya ya madaraka katika ofisi yake.
Mbali na kupongeza kazi hiyo, pia CC ilizungumzia mgogoro wa Tanzania na Malawi. Kuhusu hilo, Nape alisema Kamati Kuu imewatahadharisha wanasiasa na vyombo vya habari vinavyochochea vita na uhasama kati ya nchi hizo mbili.
“Kamati Kuu imetaka suala hilo kuiachia diplomasia ichukue mkondo wake na Serikali iushughulikie na kuumaliza mgogoro huo,” alisema Nape.
Pia, ilipokea taarifa ya maendeleo ya uchaguzi ndani ya chama na kusema imeridhishwa na maendeleo hayo ya uchaguzi na kuagiza kila kikao husika kihakikishe haki inatendeka hasa katika uchujaji wa majina.

Apple yaipiku Samsung mahakamani

Apple yaipiku Samsung mahakamani

Na Mashirika Ya habari

Jopo la mahakama moja ya Marekani limeamua kuwa kampuni kubwa ya teknolojia ya Korea Kusini, Samsung, iliiga baadhi ya ufundi mpya wa kampuni ya Marekani ya Apple kuunda simu zake wenyewe za kisasa za smartphone na kumputa ndogo - tablet.
Simu za Apple na Samsung
Baada ya kesi iliyoendelea kwa mwaka mzima, ambayo ilichunguza mashtaka kama 700 ya aina ya ufundi ulioigwa, mahakama ya California yaliiamrisha Samsung iilipe Apple fidia ya dola zaidi ya bilioni moja.
Samsung imelalamika kuwa Apple inajaribu kuhodhi soko zima la smartphone, na imesema itakata rufaa.
Zaidi ya nusu ya simu za smartphone zinazouzwa duniani ni ama za Apple au Samsung, na kampuni hizo mbili zinashtakiana katika mahakama ya nchi mbali mbali duniani.

Sunday, August 26, 2012

DC NYASA APIGA MARUFUKU WANAOOGA UCHI KANDOKANDO YA ZIWA NYASA



 DC NYASA APIGA MARUFUKU WANAOOGA UCHI KANDOKANDO YA ZIWA NYASA

Na Muhidin Amri,
NYASA

MKUU wa wilaya mpya ya Nyasa mkoani Ruvuma Ernest Kahindi, amepiga marufuku watu kuoga wakiwa uchi kando kando ya ziwa Nyasa kwani tabia hiyo imekuwa ikiwadhalilisha  wanawake na watu wazima.

Kahindi amelazimika kuchukua hatua hiyo,kufuatia kuongezeka kwa idadi kubwa ya watu siku hadi siku wanaokwenda kuonga  wa ziwani wakiwa utupu(uchi) jambo ambalo ni kinyume na utu wao na wakati mwingine kuleta matamanio kwa wenzao, na kusababisha  kuongezeka kwa vitendo vya ngono uzembe hivyo kuchangia ongezeko kubwa la maambukizi mapya ya ukimwi.

Alisema,tabia hiyo haiwezekani hata kama ni jambo la kawaida kwa wenyeji na wakazi wa ziwa ilo, na siyo kitu chenye sifa kwa mtu mzima kuvua nguo na kuoga mbele za watu na wakati mwingine  mbele ya watoto wako bila kujali aina ya jinsia ya watoto au watu hao.

"hii tabia kuanzia sasa nazuia watu kuendelea kuonga wakiwa uchi tena mbele ya kadamnasi mtu mzima unavuoa nguo ukiwa na watoto wako sijui unapata raha gani,hakuna kabila lolote lenye tabia hii hapa mimi natoka kanda ya ziwa lakini sijwahi kuona watu wakijiachia kiasi hiki"alisema.

Alifafanua kuwa,siyo kwamba anazuia watu kuoga ziwani,isipokuwa ni lazimakuwe na maeneo maalumu ya kufanyia shughuli hiyo na maeneo hayo yatenganishwe kati ya wanaume na wanawake tofauti na ilivyo sasa ambapo idadi kubwa ya watu hao wamekuwa wakioga sehemu moja au inayokaribiana kitu ambacho ni hatari na siyo cha ustaarabu kwa Watanzania.

Kahindi alitumia nafasi hiyo kuwaomba radhi wakazi wa Nyasa  kutokana na usumbufu watakaoupata, hata hivyo  alisema hali  hiyo itasaidia sana kujenga kizazi chenye maadili na kuanza kukubali mabadiliko mbalimbali yanayokuja baada ya kuwa wilaya kamili tofauti na siku za nyuma ambapo Wilaya hiyo ilikuwa kama sehemu ndogo na hakukuwa na idadi kubwa ya watu.

Alitaka kuongeza kasi ya uwajibikaji kwa kila mmoja katika kukabiliana na kasi ya maendeleo ili apo baadaye wasije kuwa vibarua kwa wageni walioanza kuingia kwa wingi  wilayani Nyasa kwa ajili ya kutafuta maisha huku wenyeji wakiridhika na kipato kidogo wanachopata kutokana na uvuvi.

Juu ya zoezi la sensa lililoanza jana nchini kote,Kahindi aliongeza kuwa zoezi ilo linaendelea vizuri na amefurahishwa na hali ya utulivu  na idadai kubwa ya watu walioshiriki kuhesabiwa na kutoa wito kwa watu ambao bada hawajahesabiwa kutoa kila aina ya ushirikiano kwa makarani wa sensa.


Aliwaonya watu watakajaribu kutaka kuvuruga zoezi ilo wasifikirie kufanya hivyo kwani serikali kupitia jeshi la polisi imejipanga kikamilifu kuwashughulikia watu hao kwani wanaweza kuleta madhara kwa wengine waliokuwa tayari kushiriki sensa ya watu na makazi.

                                          MWISHO

BAADA YA WACHIMBA MADINI KUUAWA AFRIKA KUSINI WAANZA KURUDI KAZINI

Wachimba migodi waanza kurudi kazini

Kampuni ya migodi iliyokuwa chanzo cha mgomo wa ghasia Afrika Kusini, Lonmin, inasema kuwa wafanyakazi wake zaidi wamerudi kwenye mgodi wa Marikana, karibu na Rustenberg.
Polisi nje ya mgodi wa Marikana wakati wa mgomo
Juma lilopita wachimba migodi 34 waliogoma walipigwa risasi na polisi na kuuwawa, na kama 70 walijeruhiwa.
Serikali ya Afrika Kusini imeteua tume ya majaji kuchunguza kilichotokea.
Lonmin inasema kuwa katika mgodi wa Eastern Shafts, huko Marikana, 57% ya wachimba migodi wako kazini Jumamosi.
Sehemu nyengine ya machimbo imefungwa kwa sababu ya mapumziko ya mwisho wa juma.
Kampuni inasema hali ni ya amani, na kwamba mazungumzo yanaendelea ili kushawishi wafanyakazi wote warudi kazini.
Lakini uchimbaji wa madini ya dhahabu nyeupe, platinum, ulisimamishwa kwenye mgodi huo zaidi ya majuma mawili yaliyopita kwa sababu ya mgomo, na bado kazi haikuanza.
Mazishi ya baadhi ya wachimba migodi waliokufa yamefanywa na mawaziri walihudhuria na kuahidi kuzisaidia familia za wachimba migodi hao.
Wakuu sasa wamethibitisha kuwa kati ya waliokufa, watano walikuwa wageni kutoka nchi za nje.

GAMBIA YANYONGA WAFUNGWA TISA

 Na Mashirika ya habari
Shirika la kimataifa la kutetea haki za kibinaadamu, Amnesty International, linasema limeambiwa kwamba Gambia imewanyonga wafungwa tisa kati ya 47 ambao wamehukumiwa kifo.
Rais wa Gambia, Yahya Jamme

Msemaji wa Amnesty, Lisa Sherman Nichols, aliiambia BBC kwamba wafungwa hao ni wa mwanzo kunyongwa nchini Gambia kwa miaka 29, na inasemekana alikuwako mwanamke kati yao, na wananchi watatu wa Senegal.
"Tumepata taarifa za kuaminika kuwa watu 9 walinyongwa jana usiku.
Nimezungumza na baadhi ya jamaa zao, ambao bila ya shaka wako kwenye majonzi, na wametuomba tuchukue hatua.
Wamegusia kuwa kuna wengine watanyongwa leo usiku.
Tunajaribu kuzitawanya habari hizi ulimwenguni na serikali ya Gambia inafaa kujua kuwa macho ya ulimwengu na serikali za nchi za nje yameelekezwa juu ya nchi hiyo."
Hapo awali, shirika la raia la nchi hiyo lilimlaumu rais wa Gambia, Yahya Jammeh, na lilisema kwamba wengi waliohukumiwa kifo ni wafungwa wa kisiasa.

WAHALIFU WA KICHINA WAKAMATWA ANGOLA

Wahalifu wa Kichina wakamatwa Angola


 Na Mashirika ya habari

Raia 37 wa Uchina wamerejeshwa nyumbani kutoka Angola, ambako walikamatwa kwa tuhuma za kufanya uhalifu dhidi ya Wachina wenzao.
Wahalifu wa Kichina wakiwasili kwao kutoka Angola
Uhalifu huo ni pamoja na utekaji nyara, kunyang'anya watu pesa, wizi kwa kutumia silaha, na kulazimisha wanawake wauze miili yao.
Kikosi maalumu cha polisi wa Uchina kilitumwa Angola kushirikiana na polisi wa huko dhidi ya magenge ya Wachina yaliomo Angola.
Wizara ya Uchina ya usalama inasema magenge 12 yalivunjwa.
Wizara hiyo ilisema hii ni mara ya kwanza kwa polisi wa Uchina kufanya msako mkubwa kama huo dhidi ya wahalifu wa Kichina katika bara la Afrika.

KUTENGULIWA MATOKEO IGUNGA,MAKADA WA CCM WAMNYOSHEA KIDOLE MKAPA

 
Sunday, 26 August 2012 09:34


KITENDO cha Mahakama Kuu Kanda ya Tabora kutengua matokeo ya ubunge Jimbo la Igunga yaliyompa ushindi Dk Dalaly Peter Kafumu (CCM), kimeibua mvutano mwingine ndani ya CCM, ambapo sasa  baadhi ya makada wake wameanza kumnyooshea kidole Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na baadhi ya mawaziri kuwa ndiyo chanzo cha kushindwa huko. 
Baadhi ya makada maarufu na wenye uzoefu wa muda mrefu ndani ya chama hicho tawala, kwa nyakati tofauti kwenye mahojiano na Mwananchi Jumapili wamekiri kwamba, imefika mahali ambapo CCM inapaswa ijitazame na kuwa makini juu ya watu inaopaswa kuwatumia katika  kampeni zake. 
Katika tathmini yao, makada hao wamemtaja Rais Mstaafu Mkapa na mawaziri kadhaa, wakisema kuwa CCM haikuwa makini katika kuwateua wasimame kwenye majukwaa kupiga kampeni za kisiasa.  Walitaja moja ya sababu kuwa ni Mkapa na baadhi ya mawaziri hao mashuhuri kuwa siyo wanasiasa wa jukwaani bali ni watendaji.
Licha ya CCM kujaribu kumtumia rais huyo mstaafu na mawaziri hao kutokana na heshima iliyojengeka kwao mbele ya Watanzania walio wengi, tathmini ya makada hao inaeleza kuwa hoja zao katika kampeni ama ziliwapa mwanya wapinzani, hasa Chadema kuiumbua CCM kwenye propaganda za majukwaani, hata kisheria.  
Walikuwa wakizungumzia chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibuni katika Jimbo la Arumeru na ule wa Igunga Oktoba mwaka jana, ambao licha ya CCM kushinda, wiki hii mahakama kuu ilitengua ushindi huo.  Kuanguka Igunga  Dk Kafumu aliibuka mshindi kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika Oktoba 2, mwaka jana kuziba nafasi ya Rostam Aziz aliyejiuzulu kwa madai ya kuchoshwa na kile alichoita siasa za majitaka  ndani ya CCM, lakini mahakama imetengua ushindi wake. 
Uchaguzi huo ulikuwa wa ushindani mkubwa kati ya Dk Kafumu na aliyekuwa mgombea wa Chadema, Joseph Kashindye ambaye aliamua kupinga ushindi wa Dk Kafumu mahakamani akidai hakuridhishwa na mwenendo wa uchaguzi huo.  Kashindye alifungua kesi hiyo Machi 26, mwaka huu.  Wakati wa kampeni za uchaguzi huo vigogo mbalimbali wa CCM akiwamo Mkapa walipiga kambi Igunga na kushiriki mikutano mbalimbali ya kampeni, ambapo pamoja na mambo mengine walitoa kauli tata zilizosababisha CCM kushindwa katika kesi hiyo. 
Mbali na Mkapa viongozi wengine waliotoa kauli hizo na sasa wananyooshewa vidole ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama na Mbunge wa Tabora, Ismail Aden Rage.   Kauli tata ya Mkapa  Wakili wa mlalamikaji, Profesa Abdallah Safari, Agosti 20 mwaka huu aliwasilisha mahakamani hapo zaidi ya malalamiko 13 dhidi ya Dk Kafumu na wenzake. 
Mbali na kueleza yaliyozungumzwa na Dk Magufuli, Profesa Safari alidai hoja nyingine ni Baraza la Waislamu (Bakwata) Wilaya ya Igunga kuwakataza waumini wasiipigie kura Chadema na kwamba naye Rais Mstaafu Benjamin Mkapa alitoa ahadi ya kugawa mahindi kwa wananchi wa Igunga siku moja kabla ya uchaguzi ili waichague CCM.  Makada waonya

Mbunge wa Kahama, James Lembeli alisema kuwa utaratibu wa sasa wa chama hicho kuwatumia viongozi wastaafu umepitwa na wakati kwa sababu Watanzania wa sasa hawahitaji kusikia maneno mengi, bali sera.  Alisema kuwa CCM inatakiwa itazame ilipojikwaa na kuacha kutafuta mchawi kwa kuwa matatizo yaliyokifikisha chama hicho kilipo sasa yanajulikana. 
“Kampeni za CCM hivi sasa hazina maandalizi, kila anayeweza kuzungumza anachukuliwa na kujumuishwa kwenye kampeni, jambo ambalo siyo sahihi,” alisema Lembeli na kuongeza:  “Inatumia watu bila kuangalia kama wanakubalika, katika chaguzi zinazokuja, chama kiwatumie  makada wanaopendwa na wananchi na wenye uwezo wa kuuza sera za chama.” 
Alitaja sababu nyingine ya CCM kuanguka hasa Igunga kuwa ni pamoja na mgawanyiko uliokuwapo ndani ya chama hicho baada ya baadhi ya makada kuzuiwa kushiriki katika kampeni hizo wakati wana mvuto kwa wapiga kura.  Akitolea mfano watu hao alisema kuwa ni pamoja na Mbunge wa Urambo Mashariki, Samuel Sitta, ambapo alibainisha kuwa waliotoswa katika kampeni hizo wasingeweza kuishiwa maneno ya kuzungumza na kuanza kutoa ahadi zinazovunja sheria ya uchaguzi.
Dk Kigwangallah Akizungumzia suala hilo, Mbunge wa Jimbo la Nzega, Dk Hamisi Kigwangallah alisema kitendo cha CCM kutumia vigogo akiwamo Rais mstaafu Mkapa katika uchaguzi wa Igunga, ndiyo chanzo cha kushindwa kwa kesi hiyo kwa kuwa walizungumza mambo yasiyo na msingi wowote.  Dk Kigwangallah ambaye Agosti 22 alichukua fomu za kuwania kiti cha Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa alisema kuwa uchaguzi mwingine ukifanyika katika jimbo hilo, viongozi na wabunge kutoka mikoa ya Tabora, Mwanza na Shinyanga ndiyo waachwe kufanya kampeni.
“Ni kweli CCM tuliweka watu wengi, ambao walipunguza kura za chama, lakini pia walizungumza mambo yasiyostahili,” alisema Dk Kigwangallah na kuongeza:  “Uchaguzi ujao Igunga wasituletee watu kutoka CCM taifa, wanakuja na helikopta na kutumia gharama kubwa halafu mambo yanaharabika. Nadhani tubadilishe hali hii.”
Hata hivyo, alisema kuwa CCM inakubalika kwa kiasi kikubwa mkoani Tabora, hasa katika Jimbo la Igunga na kwamba kama Dk Kafumu akigombea tena, ataibuka mshindi kwani anakubalika na alishafanya mambo ya maendeleo. 
Ibrahim Kaduma Kada mkongwe wa chama hicho, Ibrahim Kaduma alipoulizwa iwapo moja ya sababu za CCM kushindwa ni kuwatumia vigogo ambao siyo mahiri katika siasa za jukwaani, hakuwa tayari kulizungumzia suala hilo akitaka aachwe.  “Naomba uniache kwanza, masuala haya yanatosha …, naomba uniache tafadhali kwa hisani yako tu,” alisema Kaduma.  Ole Moloimet  Naye Lepilal Ole Moloimet, kada wa CCM aliyewahi kushika nafasi mbalimbali ndani ya CCM na Serikali, alikilaumu chama chake kwa tabia ya kumtumia Rais Mstaafu Mkapa na baadhi ya mawaziri kwenye kampeni za uchaguzi. 
Alisema kitendo cha kuwatumia watu hao licha ya kusababisha wadhalilike kinaonyesha udhaifu wa watu wanaoiongoza CCM hivi sasa.  "Suala la kuwatumia marais wastaafu, kuwatumia mawaziri ni udhaifu wa viongozi wa CCM wanaoiongoza hivi sasa," alisema Moloimet.  Akizungumzia  uchaguzi wa Arumeru alisema: “Mkapa alidhalilishwa na mgogoro wa ardhi wa muda mrefu. …Wananchi walihoji kama alishindwa mgogoro huo wakati wa utawala wake, akizungumzia suala hilo sasa atakuwa anawaongopea."
Alisema kimsingi marais wastaafu hawapaswi kutumiwa kwenye siasa, badala yake iwe ni matukio muhimu yanayohusu Watanzania wote au juu ya uhusiano wa kimataifa kama vile mgogoro wa mpaka na Malawi.  "Imefika mahali hawa viongozi wastaafu hata  wakiombwa wakanadi sera majukwaani wao wenyewe wanapaswa wajipime. Si kila kitu wakubali," alisema Moloimet.   
Tuvute subira- Mgeja  Hata hivyo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja alisema: “Nadhani tuvute subira kwa sababu tukianza kunyoosheana vidole nani hakufaa nani alifaa itakuwa siyo jambo zuri, kama ni hivyo mbona tulivyoshinda Igunga hawakuwalaumu walioshiriki katika kampeni.”  
Lusinde: Hakuna tatizo
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde alisema kuwatumia wazee katika chaguzi za chama hicho hakuna tatizo, akiamini kuwa Jimbo la Igunga ni mali ya CCM na kwamba uamuzi wa kukata rufaa au kutokata anamwachia Dk Kafumu.  “Natamani kama uchaguzi ungefanyika tena ili twende tukalichukue jimbo,” alisema Lusinde.
Sababu za kutenguliwa matokeo  Akitoa hukumu hiyo, Jaji Mary Nsimbo Shangali alisema Mahakama ilipokea malalamiko 15 ambayo yaliridhiwa na pande zote mbili lakini baadaye yakaongezwa madai mengine mawili hivyo kufikia 17.  Alisema hoja zilizothibitishwa na Mahakama ambazo  zilizotumika kutengua matokeo hayo ni saba kati ya 17. 
Baadhi ya hoja hizo ni pamoja madai kwamba Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli alitumia nafasi yake ya uwaziri kutoa ahadi ya ujenzi wa Daraja la Mbutu, ambalo lilikuwa ni moja ya kero kubwa kwa wananchi wa Jimbo la Igunga.  Jaji Shangali aliikubali hoja nyingine ya washtaki kuwa ni ugawaji wa mahindi ya kuwawezesha wakazi wa Igunga kukabiliana na njaa wakati wa uchaguzi huo kwamba ulitumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa kuwashawishi wananchi wawapigie kura.
Mbali na Dk Kafumu, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ya uchaguzi walikuwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Igunga aliyetangaza matokeo hayo.    
Kauli ya Nape  Hata hivyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alipoulizwa kwamba haoni kuwa kauli za Rais Mkapa, Magufuli, Mukama ndizo zilizokiangusha chama hicho alisema: “Ndiyo maana tunataka kukata rufaa kwa sababu hatukubaliani na hiyo hoja.”
Vita ya kuwania uongozi
Katika hatua nyingine, upepo wa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM umezidi kushika kasi baada ya Mbunge wa Jimbo la Kahama, James Lembeli kuchukua fomu ya kugombea Uenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga huku akitamba kuwa ameingia kwa lengo la kumaliza makundi ya kisiasa yaliyokithiri ndani ya chama hicho. 
Lembeli amechukua fomu sambamba na mpinzani wake mkubwa kisiasa Khamis Mgeja, ambaye kwa sasa ndiye mwenyekiti wa CCM mkoani humo.  Mbali na vigogo hao, mbunge wa zamani wa Shinyanga mjini Leonard Derefa naye alichukua fomu za kuwania nafasi hiyo.
Wengine ni Teresia Kashinje, Bonaventure Mguziki, Regina Masanja na Alex Seseja.   Hata hivyo, katika kinyang’anyiro hicho wagombea wanaoonyesha kuvutia  hisia za wanaCCM wa Shinyanga ni Lembeli na Mgeja, ambao wamekuwa mahasimu wa siku nyingi katika siasa za mkoa huo, huku wote wakitoka wilayani Kahama.
Katika majigambo yao Lembeli amekuwa akinukuliwa na vyombo vya habari akitamba kuwa atahakikisha anamng’oa Mgeja katika nafasi hiyo huku Mgeja naye akidai hasimu wake huyo ni ‘sisimizi’ ambaye hamnyimi usingizi.
Makada wengine wa chama hicho waliochukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali ni pamoja na  Mkurugenzi wa Uchaguzi CCM Makao Makuu, Matson Chizii ambaye amejitosa kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Chama Mkoa wa Dar es Salaam.  Wengine waliochukua fomu za kuwania nafasi hiyo mkoani Dar es Salaam ni  John Guninita anayetetea nafasi hiyo na Mjumbe wa Nec, Ramadhan Madabida.

Naye Katibu wa Nec, Uchumi na Fedha na Mbunge wa Iramba  Magharibi, Mwigulu Nchemba amejitosa kuwania nafasi ya mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (Nec) kupitia kundi la viti 10 wakati Mbunge wa Mchinga, Said Mtanda akijitosa kuwania nafasi ya NEC kupitia Wilaya ya Lindi Vijijini.  Aliyekuwa mbunge wa Misungwi, Dalali Shibiriti naye amechukua fomu ya kuwania Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) kupitia wilaya hiyo. 
Uchaguzi huo pia umemwibua aliyekuwa Mbunge wa Busega, Dk Raphael Chegeni ambapo baadhi ya vijana wa wilaya hiyo walimchukulia fomu kuwania Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kupitia Wilaya ya Busega.  Mbunge wa Jimbo la Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi naye amejitosa kuwania nafasi ya uenyekiti wa mkoa wa chama hicho mkoani Mbeya.

MADIWANI NA WATENDAJI WA ASERIKALI WATAKIWA KUJIBU KERO ZA WANANCHI



Na Muhidin Amri
Songea
MKUU wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu amewataka watendaji wa serikali,na madwani mkoani humo kujibu na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Mwambungu aliyasema jana ofisini kwake mjini songea wakati akizungumza na na Mtandao huu kuhussiana na ochangamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa mkoa huo.

Alisema wananchi wanamatarajio makubwa ya kuona hali ya maisha yao yanabadilika hasa baada ya Rais Jakaye Kikwete kufanya mabadiliko makubwa serikalini ikwemo ya kulibadili baraza la mawaziri na makatibu wakuu wa wizara mbali mbali.

Mwambungu alisema wananchi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazowakabili kila siku ambazo zinapaswa kupatiwa majibu ni kazi ya watumishi wanazipatia majibu chaangamoto hizo na kuhakikisha wanafuatilia kwa ukaribu shughuli zote za kimaendeleo zinazofanyika.

Alitolea mfano suala la pembejeo za ruzuku ambalo limekuwa katika baadhi ya maeneo likilalamikiwa ma wananchi pengine kutokana na kutotekelezwa vyema na baadhi ya mawakala hivyo sasa linapaswa kusimamiwa kwa ukaribu zaidi ili kuepusha malalamiko.


Mkuu huyo wa mkoa aliwataka wananchi wa mkoa huo kushirikiana na viongozi wao katika kujiletea maendeleo na kwamba wajitokeze kwa wingi katika kuchangia nguvu zao kwenye ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili hatimaye iweze kuwanufaisha wao wenyewe.

                            MWISHO.

MWANAMKE ALIYEMTUMPA MTOTO WAKE JALALANI ATIWA MBARONI


MWANAMKE ALIYEMTUMPA MTOTO WAKE JALALANI ATIWA MBARONI

Na Cresensia Kapinga
Songea
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma limemtia mbaroni mwanamke aliyedaiwa kutupa mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miezi mitano kwenye jalala la takataka lililopo katika eneo la mtaa wa Majengo katika halmashauri ya manispaa ya Songea. 

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani humo Deusdeti Nsimeki alisema kuwa mwanamke Zawadi (18) wa mtaa wa Majengo alikamatwa juzi  majira ya saa za usiku kwenye nyumba ya kulala wageni akiwa amejificha uvunguni mwa kitandaakiwa analengo la kuukimbia mkono wa dola.

Kamanda Nsimeki alisema kuwa Bi. Zawadi baada ya kukamatwa na kuhojiwa kuwa kwa nini aliamua kumtupa mtoto na kukimbia alisema kuwa alikuwa amedanganywa na mwanaume ambaye hakumtaja jina kuwa amtupe mtoto alafu wafunge ndoa kisha waende Mbeya wakaendelee na maisha yao.

Alieleza zaidi kuwa awali alipohojiwa na polisi alisema kuwa alikuwa anakimbizwa na kichaa kitendo ambacho kilimfanya amtupe mtoto wake lakini alipobanwa zaidi ndipo alipokiri na kubainisha zaidi kuwa alikuwa ameingia kwenye dimbwi la mapenzi ambalo alidai kuwa angefanikiwa kumtupa mtoto wake maisha yake ya ndoa yangekuwa mazuri zaidi.

Alifafanuwa zaidi kuwa Polisi baada ya kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo badinaendelea kufanya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo na kwamba hali ya mtoto inaendela kuwa nzuri na hivi sasa kuna msamaria mmoja amejitokeza kumlea.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani wakati wowowte kuanzia sasa mara tu upelelezi utakapokamilika ili sheria iweze kuchukuwa mkondo wake.

MWISHO.

Saturday, August 25, 2012

CCM IRINGA KUPELEKA CHUONI KUPATA MAFUNZO ELEKEZI MAKADA WAKE KWENYE CHUO CHAKE

 Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa Bw. Emanuel Mteming'ombe
 Bw. Mteming'ombe

 
Na Joseph Mwambije,
Iringa
CHAMA  cha Mapinduzi(CCM) Mkoani Iringa kinatarajia kupeleka Makatibu Kata 93 wa chama hicho waliochaguliwa hivi karibuni  kupata  Mafunzo elekezi  ya utendaji kwenye Chuo cha chama hicho Mkoani humo  ili kuondoa migogoro ndani ya Chama hicho.
 
Hayo yalibainishwa hivi karibuni na Katibu wa Chama hicho wa Mkoa wa Iringa Bw. Emmanuel Mteming’ombe wakati akizungumza na Mtandao huu Mkoani humo.
 
Alisema Ukarabati wa Chuo hicho umeshakamilika na Wanatarajia kupeleka Makada Chuoni hapo kupata mafunzo ya wiki moja kuanzia Septemba 3 hadi Septemba 10 mwaka huu.
 
Katibu huyo wa CCM alisema hatua hiyo inalenga kuwapatia mafunzo elekezi  Viongozi wa Kata waliochaguliwa hivi karibuni katika chenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 200 kwa mara moja.
 
‘Tunalenga kuwapatia mafunzo makatibu wapya  ili wajue kazi za utendaji wa Chama ili waweze kukijenga Chama na baada ya mafunzo hayo tutatoa mafunzo mengine kwa Makatibu wa Matawi kwenye Wilaya zote za Mkoa wa Iringa’alisema Bw. Mteming’ombe.
 
Alifafanua kuwa Makatibu hao wa Kata wote ni wa kutoka katika Mkoa huo wa Iringa na baadaye kutafuatiwa na  mafunzo mengine  kwa  Makatibu wa Matwi toka  Wilya ya Njombe yatakayoanz Oktoba 3 hadi Oktoba 10 mwaka huu.
 
Bw. Mteming’ombe anafafanua kuwa mafunzo kwa Makatibu Kata yanatarajiwa kufunguliwa Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama hicho,Mbunge wa Jimbo la Isimani na Waziri wa Sera na Uratibu wa Bunge Bw. Wiliam Lukuvi.
MWISHO
 

 Jengo la CCM Mkoa wa Iringa
Jengo la CCM  Mkoa wa Iringa.

WAKULIMA WAWEZESHAJI NJOMBE NA RUVUMA WAPATIWA MAFUNZO YA KILIMO BIASHARA

 Wakulima wakiwa kwenye mafunzo hayo yaliyoandaliwa na MVIWATA na kudhaminiwa na Shirika la chakula duniani(FAO).Jumla ya Wakulima 50 wa Mikoa ya Njombe na Ruvuma wamenufaika na mafunzo hayo yanayotolewa kwa awamu ya nne na kufanya jumla ya wakulima 200 kunufaika na mafunzo hayo.
 Mwezeshaji wa mafunzo hayo Bi. Silla Richard akiwaeleza wakulima namna ya kufanya kilimo biashara.Baada ya kuhitimu mafunzo hayo wakulima hao wanatakiwa kwenda kuwafundisha wakulima wenzao namna ya kufanya kilimo biashara.
 Afisa  akiba na mikopo wa Mtandao wa Vikundii vya  vya  wakulima Tanzania(MVIWATA) Bw. Julius Mahula akifundisha kwenye mafunzo hayo.
 Baadhi ya Wawezeshaji wakifuatila mambo kwenye mafunzo hayo ya siku tatu.Wa pili kulia ni Mratibu wa MVIWATA Mkoa wa Ruvuma Bw. Ladslaus Bigambo
 Bw. Mahula akisisitiza jambo
 Bi. Silla akifundisha kwa kutumia picha
 Akizungumza na wakulima hao namna ya kukifanya kilimo kuwa cha manufaa.
 Mkulima kutoka Kijiji cha Kitanda Namtumbo Bw. Joseph Kilowoko akisisitiza hoja kwa wenzake. 
Profesa Neka akiwachangamsha wenzake kwenye mafunzo hayo.

Wednesday, August 22, 2012

MWANASHERIA WA CCM AJITOSA KUGOMBEA UNEC KUPITIA WILAYA YA SONGEA VIJIJINI

 Mwanasheria wa CCM Bw. Glorious Luoga akipokea fomu za kugombea ujumbe wa Halmashauri kuu Taifa(NEC)katika Chama cha Mapinduzi toka kwa Katibu wa CCM Songea Vijijini  Bi. Lyidia Gunda.
 Akishukuru toka kwa Katibu huyo baada ya kupokea fomu hizo.
 Akitoa maelezo kwa Katibu.

 Akiwa ametoa fedha za kuchangia Chama hicho na fza fomu.
 Akihesabu fedha za kuchangia Chama hicho kabla hajazitoa.
 Akitoa fedha aa kuchangia Chama kiasi cha shilingi laki moja.
 Aliondoka baada ya zoezi hilo.Mwanasheria huyo amebainiasha kuwa Chama hicho kupitia kwenye misukosuko ndio kuimarika kwake.
 Akizungumza baada ya zoezi la kupokea fomu na kuchangia Chama na kusema anaomba kutumwa kwenda anakokujua ili akivushe Chama hicho katika kipindi hiki kigumu.Kulia ni mama yake mzazi aliyemsindikiza kwenda kuchukua fomu Bi. Antonia Mselewa Diwani wa Viti maalumu Kata ya Madaba.
 Akiendelea kujinasibu kwamba amekuja kuwapokea mkongojo wazee ili kuyaendeleza yale waliyoyaanzisha na kubainisha kuwa tayari amekwishakisaidia chama kutimiza wajibu wake akiwa Mwanasheria wa chama hicho kwa kushinda kesi zote alizozisimamia.
Waandishi wa Vyombo mbalimbali vya habari wakikava Story ya Mwanasheria huyo kuchukua fomu.