Tuesday, June 11, 2013

KAMPUNI YA VODA COM TANZANIA YAZINDUA MRADI WA MWEI (M-PESA WOMEN EMPOWERMENT INITIATIVE – SONGEA MKOANI RUVUMA

 Mkuu wa Wilaya Songea Joseph Mkirikiti akizungumza na akina mama wajane wa Manispaa ya Songea wakati wa uzinduzi  wa mradi wa MWEI (M-Pesa Women Empowerment Initiative) katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa wilaya
 Meneja wa Voda Com Fonundation Mwamvua Mlangwa akimpa maelekezo namna ya kujaza fomu za maombi ya mkopo Grace Kienyi mkazi wa kata ya Lilambo
 Washiriki wakijaza fomu za maombi ya mkopo
Kutoka kushoto ni Meneja wa Voda Com Fonundation Mwamvua Mlangwa akiteta jambo na Meneja mawasiliano wa Voda Com Rukia Mtingwa
 Mwandishi wa habari wa kituo cha ITV mkoa wa Ruvuma Bw. Nathan Mtega akisalimiana na Meneja mawasiliano wa Voda Com Rukia Mtingwa wakati wa uzinduzi wa mradi wa MWEI (M-Pesa Women Empowerment Initiative) mkoani Ruvuma.
Hawa ni miongoni mwa mama wajane waliojitokeza wakisikiza kwa makini maelekezo ya mkopo wa mradi wa MWEI (M-Pesa Women Empowerment Initiative)
 Meneja wa Voda Com Fonundition Mwamvua Mlangwa akiwaelezea akina mama wajane  masharti ya mkopo wa mradi wa MWEI (M-Pesa Women Empowerment Initiative)
Meneja mawasiliano wa Voda Com Rukia Mtingwa akijaribu kuwafafanulia maana halisi ya neno mjasiriamali kwa akina mama wajane ambao ni wajasiriamali waliohudhulia katika uzinduzi wa mradi wa MWEI (M-Pesa Women Empowerment Initiative) 
---------------------------------------------------------
Kampuni ya VodaCom Tanzania Limited kupitia kitengo chake cha huduma kwa jamii(Voda Com Fonundation) imebuni mradi wa MWEI (M-Pesa Women Empowerment Initiative) unaotumia huduma ya mpesa kuwapatia mikopo isiyo na riba akina mama wanaoishi katika maeneo ya vijiji.

Mradi huu ni mkakati wa kampuni ya Vodacom katika kusaidia juhudi za Serikali za kupiga vita umasikini hapa nchini. Mradi wa MWEI unalenga kuwaongezea  uwezo wa kiuchumi (Mitaji) akina mama wanaojishuhulisha na shughuli mbali mbali kwa lengo la kujipatia kipato.

Naye Meneja wa Voda Com Fonundition Mwamvua Mlangwa akisoma risala amesema mradi huu ulizinduliwa rasmi na Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Kayanda Pinda mwezi Julai 24. 2011 ambapo mpaka sasa umeshawafikia wakina mama zaidi ya 7000 Tanzania Bara na visiwani.

Kwa upande wa mkoa wa Ruvuma katika bajeti ya mwaka huu mradi huu unatarajia kuwanufaisha  akina mama 400 katika vijiji vya Peramiho, Muhukulu na Kigonsera.

 Akizungumza kabla ya kuzindua mradi huo Mkuu wa wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti mbali ya kuishukuru kampuni hiyo ya simu za mkononi kwa kuwakumbuka akina mama wajasiriamali ambao ni walezi wakubwa wa familia lakini pia aliwaasa akina mama hao kuitumia fursa hiyo ipasavyo.

Pia amesema kuwa zipo taasisi na kampuni mbalimbali ambazo zimekuwa zikitoa mikopo huku ikiwa na mashariti magumu, riba pamoja na gharama za uendeshaji ambayo yamekuwa hayatoi fursa kwa baadhi ya makundi wakiwemo akina mama lakini imekuwa tofauti kwa kampuni ya simu ya mkononi ya voda Com kwa kupitia mradi huu wa kuwajengea uwezo akina mama wajasiliamali bila masharti magumu wala riba.

Aidha amesema kuwa serikali ya wilaya itahakikisha kuwa programu hiyo inakuwa endelevu kwa ajili ya kuwanufaisha akina mama wajasiliamali ambao ndiyo nguzo ya familia zao ambazo wanazilea bila kujali 

CHANZO-DEMASHO  BLOG

Friday, June 7, 2013

RASIMU YA KATIBU MPYA :MAWAZIRI KUKAIMU URAIS

.Ni mapendekezo ya Rasimu ya katiba mpya


  Makamu wa Rais Dkt Gharib Bilali akionyesha Rasimu ya Katiba mpya kabla ya kuizindua Jijini Daressalaam.Wa kwanza  kulia ni Waziri Mkuu wa Tanzania,Mizengo Pinda.Wa kwanza  kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya  Joseph Warioba na anyemfuatia ni Makamu wa kwanz wa Rais Zanzibar Seif Sharif .

HABARI KAMILI......

 Kutokana na rasimu ya Katiba Mpya kupendekeza kufutwa kwa nafasi ya Waziri Mkuu, rasimu hiyo inapendekeza waziri yeyote mwandamizi ateuliwe kukaimu nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa rais na makamu wake hawapo nchini kutokana na sababu zozote zile.
Mapendekezo hayo ni tofauti na Katiba ya sasa ambayo inatamka kwamba ikiwa Rais na Makamu wake hawapo, basi nafasi hiyo ya juu katika nchi itashikwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri Mkuu aliwekwa katika orodha ya wanaoweza kukaimu nafasi hiyo katika marekebisho ya Katiba yaliyofanywa mwaka 2000 kupitia waraka maalumu wa Serikali (white paper) na baadaye kupitishwa na Bunge.
Kabla ya marekebisho hayo ya 13, Ibara ya 37(3)(a) na (b) ilikuwa ikieleza kuwa iwapo Rais na Makamu wake hawapo nafasi hiyo ilitakiwa kushikiliwa na Spika wa Bunge na kama hayupo basi Jaji Mkuu wa Tanzania ndiye alitakiwa kukaimu nafasi hiyo.
Lakini mapendekezo ya Rasimu ya Katiba Mpya katika Ibara ya 73(1)(b)na (c) inaeleza kuwa endapo Rais na Makamu wake hawatakuwapo basi nafasi hiyo itashikiliwa na waziri mwandamizi na kama hatakuwapo basi Baraza la Mawaziri ndilo litakalokuwa na dhamana ya kuchagua mtu wa kukaimu nafasi hiyo.
Hata hivyo, mtu yeyote atakayekaimu nafasi ya madaraka ya Rais, kwa namna yoyote ile, hatakuwa na madaraka ya kuteua au kumwondoa madarakani kiongozi yeyote yule aliyeteuliwa na Rais kwa mujibu wa Katiba au jambo jingine lolote kama litakavyoainishwa na Rais katika hati ya kukasimu madaraka yake.
“Rais atakasimu madaraka yake kwa hati maalumu aliyotia saini yake,” inaelekeza rasimu hiyo iliyozinduliwa Jumatatu wiki hii na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Kadhalika rasimu hiyo inaeleza kuwa endapo Baraza la Mawaziri litaona kuwa Rais hawezi kumudu kazi zake kwa sababu ya maradhi ya mwili au akili, linaweza kuandaa azimio la kumwomba Jaji Mkuu athibitishe kwamba Rais, kwa sababu ya maradhi ya mwili au ya akili, hawezi kumudu kazi zake.
“Baada ya kupokea azimio hilo, atateua bodi ya utabibu ambayo itachunguza suala hilo na kumshauri Jaji Mkuu ipasavyo,” inaelekeza rasimu hiyo.
Jaji Mkuu baada ya kutafakari ushauri na ushahidi wa kitabibu, atampelekea Spika hati ya kuthibitisha kwamba kutokana na maradhi ya mwili au akili, Rais ameshindwa kumudu kazi zake, na iwapo Jaji Mkuu hatabatilisha hati hiyo ndani ya siku saba kutokana na Rais kupata nafuu na kurejea kazini, basi itahesabiwa kwamba kiti cha Rais kipo wazi.
Kutokana na hali hiyo, bodi ya utabibu itakayoteuliwa kwa mujibu wa Katiba itajumuisha watu wasiopungua watatu kutoka miongoni mwa madaktari bingwa wanaotambuliwa na sheria inayohusu madaktari ya Tanzania.
“Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi, kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au akili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na kushika madaraka ya Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano,” inaeleza sehemu nyingine ya rasimu hiyo.

CHANZO-MWANANCHI

RAIS KIKWETE AHITIMISHA ZIARA YA SINGAPORE KWA KISHINDO

RAIS KIKWETE AMLIZA ZIARA YA SINGAPORE KWA KISHINDO

Baadhi ya wafanyabiashara walioongozana na Rais Jakaya Kikwete katika ziara ya kikazi nchini Singapore wakiwa katika picha ya kumbukumbu na mawaziri walio katika msafara huoleo Juni 6, 2013. . Wa pili kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe akifuatiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Abdallah Kigoda na Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe (wa tatu) kulia. w2Mojawapo ya vivutio vikubwa katika jiji la Singapore ni hoteli hii ya kitalii na casino iitwayo Marina Bay ambayo kuna jengo la mgahawa  lenye umbo la meli juu ya majengo yake mawili w3 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji Upya wa Miji Upya  ya Singapore leo Juni 6, 2013 ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu. w4 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika picha ya pamoja na viongozi wa Mamlaka ya Ustawishaji Upya ya Miji ya Singapore leo Juni 6, 2013.w7 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji mijini ya Singapore leo Juni 6, 2013.ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji mijini ya Singapore leo Juni 6, 2013.ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji mijini ya Singapore leo Juni 6, 2013.ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu
w10 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika picha ya pamoja na viongozi wa Mamlaka ya Ustawishaji Upya wa miji ya Singapore leo Juni 6, 2013

Friday, February 1, 2013

MWANDISHI WA HABARI WA TANZANIA AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA KENYA


 
Kenya

MAMLAKA ya Mapato Kenya(KRA),inamshikilia mwandishi wa habari wa Tanzania kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroin kiasi cha kilo 5.436 zenye thamani ya karibu Sh234 milioni.
Mtanzania huyo ambaye aliwahi kuwa mtangazaji katika kituo kimoja cha redio nchini, alikamatwa akiwa anataka kusafirisha dawa hizo kwenda China.

 Habari zinasema kuwa, mtuhumiwa huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na raia mmoja wa Sweden, ambaye alimtambulisha kwa maofisa usalama kwamba amekuwa  akisafiri mara kwa mara katika nchi za Ghana, Kenya na Mauritius.

“Mamlaka ya Mapato Kenya inataka kutaarifu maendeleo ya sakata la kukamatwa kwa kilo 5.436 za heroin zilizokamatwa Januari 23 mwaka 2013 saa 4:40 usiku.”
“Imethibitika kuwa kilichokamatwa ni dawa aina ya heroin yenye thamani ya Sh13 milioni za Kenya…kwamba mtuhumiwa… (Jina tunalo kwa kuwa hajafikishwa mahakamani) hakuwa mwanafunzi lakini ni mtangazaji wa redio nchini Tanzania.”

Ametambulika kuwa mtangazaji wa kituo kimoja cha redio kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroin zenye thamani ya Sh234 milioni.
Mtuhumiwa huyo  alikamatwa  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kenyatta akiwa katika jaribio la kuelekea nchi za Ulaya na kwamba kukamatwa kwake kulifanikiwa kutokana na mtego ulioandaliwa na maofisa wa usalama uwanjani hapo.
Taarifa zinasema kuwa, mtuhumiwa huyo alijitambulisha kama mwanafunzi anayesoma Sweden, lakini hata hivyo ilikuja kubainika kuwa alikuwa na kibali cha ukazi alichokipata Novemba 28 na kilitazamiwa kuisha muda wake Novemba 28,2014.
Naibu Kamishna wa KRA, Kenned Onyonyi alisema kuwa maofisa wa usalama wanaendelea na uchunguzi zaidi na taarifa zaidi zitatolewa baadaye.
Habari zinasema kuwa, mtuhumiwa huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na raia mmoja wa Sweden, ambaye alimtambulisha kwa maofisa usalama kwamba amekuwa  akisafiri mara kwa mara katika nchi za Ghana, Kenya na Mauritius.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, mtuhumiwa huyo  amewahi kufanya kazi na Clouds fm akiwa kama mtangazaji mwanafunzi katika kipindi cha Leo tena na baadaye aliachana na kampuni hiyo na kujiunga na gazeti hili akiandika habari za burudani. Aliachana na gazeti hilo na kuendelea na maisha yake ya kawaida.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Kikosi cha Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Godfrey Nzowa alisema kuwa  hawajapata taarifa za kukamatwa kwa Mtanzania huyo, bali wamezisoma tu kwenye baadhi ya vyombo vya habari.
“Kuna utaratibu ambao inabidi watujulishe kwani kuna tume ya kuratibu dawa za kulevya  hivyo tunasubiri atuambie kuhusu tukio hilo,”alisema Nzowa.

CHANZO-GAZETI LA MWANANCHI

Monday, January 28, 2013

MWANAMKE MWENYE HIPS KUBWA DUNIANI APATIKANA

             .Ni Mmarekani Mikell Ruffinel


LOS ANGELES, Marekani
WAKATI wanawake wengi duniani wakihangaika kukuza ukubwa wa makalio yao, huku wengine wakitumia njia ya kuvaa taiti zenye hipsi, wanaume wengi huko mjini Los Angeles wamejikuta  wakigeukageuka kumwangalia mwanamke mwenye makalio makubwa kupita kiasi kila apitapo njiani.
Mikel Ruffinelli ni mwanamke ambaye mpaka sasa ‘ameishavunja shingo’ za wanaume wengi. Makalio yake na hispi zake za asili zimemfanya atawazwe kuwa mwanamke mwenye hipsi kubwa kuliko wanawake wote duniani.
Mikel anayeishi nchini Marekani hajatumia dawa za mchina wala dawa zozote kama wafanyavyo akina dada wengine na ndiye aliyetambulishwa kuwa ndiye mwanamke mwenye hipsi kubwa kuliko wanawake duniani. Mpaka sasa mama huyo mwenye familia yake ana  hispi zenye  mita 2.44.
Umbile lake halikuja hivihivi, bali alikuwa ni mtu mwenye umbile la kawaida, licha ya kukiri kuwa ndugu zake wengi wana maumbile makubwa.
Hipsi za mwanamama huyo zimekuwa zikiongezeka siku baada ya siku kadiri alivyokuwa akijifungua watoto wake.
Mikel Ruffinelli, ambaye ni mama wa watoto wanne ana umri wa miaka 39 na ni mkazi wa Los Angeles amejisifia kuwa umbile lake limekuwa likiwachanganya wanaume wengi.
Akiwa na kiuno kidogo kisichoendana na mwili wake cha inchi 40, hispi zake zina mzunguko mkubwa wa inchi 96.
“Nalipenda umbile langu na sina mpango wa kujikondesha kwa diet,” alinena Mikel na kuongeza kuwa wanaume wengi wanapenda wanawake wenye maumbile makubwa siyo wale wembamba wembamba.”
Lakini kauli hiyo, imepingwa vikali na Jennifer Lopez, Kim Kardashian na Beyonce ambao wanasema inategemea na mwanaume husika na namna kile anachokipenda, lakini wakati mwingine hutegemea na mazoea ya mwanamume.
Mikel pamoja na kutamba na maumbile yake hayo ambayo anadai ni urithi toka kwenye familia yake ambapo karibuni ndugu zake wote wa kike nao wana hispi kubwa.
Mikel amelazimika kuishi tofauti ili aweze kuendana na umbile lake, hawezi kuenea kwenye gari ndogo hivyo gari analoliendesha ni kama lori.
Akiwa nyumbani kwake inabidi akae kwenye makochi yaliyotengenezwa kwa chuma badala ya mbao, pia kitanda chake nacho ni futi saba kwa saba.
Mume wa Mikel, Reggie Brooks mwenye umri wa miaka 40 ameelezea kupagawishwa na umbile la mkewe na ameongeza kuwa kila siku humsifia kwa kumwambia jinsi gani alivyo mrembo.
Mikel na mumewe wapo kwenye ndoa kwa miaka 10 sasa na wamefanikiwa kupata watoto watatu ambapo mtoto wa kwanza wa Mikel alizaliwa katika ndoa yake ya kwanza kabla hajaachika na kuolewa na Reggie.
  CHANZO-GAZETI LA MWANANCHI

Sunday, January 27, 2013

MWAKYEMBE ATAMBA KUIFANYA BANDARI YA DAR KUWA YA KISASA

 
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe. 

HABARI KAMILI

WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ametamba kuifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa ya mfano duniani kwa utoaji wa huduma bora za upakiaji na upakuaji kwa wananchi wa ndani na nje ya nchi.
Hayo aliyasema jana alipokuwa akizungumza na madereva wa malori na wadau wengine wa bandari baada ya madereva hao kumtaka awasikilize kero zao wakati alipokuwa bandarini hapo na msafara wa mawaziri kutoka nchini Uganda.
Dk Mwakyembe alilazimika kurudi bandarini hapo jana baada ya juzi kuombwa na madereva hao kuonana naye ili wamweleze kero zao na yeye aliahidi kurudi kesho yake ambayo ilikuwa jana.
Katika mazungumzo hayo Waziri Mwakyembe aliwataka madereva hao kuwa wawazi kueleza kero zote zinazowakabili bandarini hapo kwa kuwa yeye hasa ndiye mwenye dhamana ya kurekebisha na kuboresha huduma bandarini.
Wadau hao walimweleza waziri kuwa kero ni nyingi zikiwamo za upatikanaji wa vibali vya upakiaji na foleni ya magari, ratiba na muda wa kupakia, mwingiliano wa kazi za meli na malori ya mizigo na madai ya rushwa kwa wafanyakazi hasa wa kitengo cha upakiaji wa makontena bandarini hapo.
Waziri aliwataka watendaji bandarini hapo kuondoa urasimu kwani hakuna haja ya malori ya kusafirisha mizigo nje ya nchi kuwa na foleni ndefu bandarini hapo kwa kuwa suala hili linapunguza ushindani wetu katika soko.
“Hakuna haja ya malori ya mizigo yaendayo nje ya nchi kuchelewa kutoka, na ndiyo sababu inayofanya Mombasa wanatuzidi kwa ufanisi” alisema Mwakyembe.
Katika kuimarisha utoaji wa huduma waziri aliwataka TICTS kufanya kazi kwa saa 24 kila siku na kwa siku saba ili kuondoa msongamano wa malori tofauti na sasa ambapo mizigo hupakiwa siku za Jumatatu mpaka Jumatano kuanzia saa 5.00 asubuhi kwa awamu tatu kwa siku kama alivyothibitishiwa na Meneja wa TICTS Bandari ya Dar es Salaam, Daniel Tawale. Akitafuta suluhu ya kero zote za bandarini hapo toka kwa wadau tofauti, waziri alisema kuwa kamati ya muda iundwe ili kwa muda wa siku saba ifanye utafiti na imshauri nini cha kufanya ili kuinusuru bandari hiyo.
“Nataka niunde kamati ndogo sasa hivi ili ichunguze na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike na inipe majibu ndani ya siku saba ofisini kwangu ili niweze kufanya uamuzi sahihi kwa kuwa ni lazima tubadilike ili tuweze kuhudumia wateja wengi wanaotuzunguka” alisema waziri wakati akiunda kamati hiyo.
Waziri aliunda kamati ndogo yenye wajumbe 10 toka sekta tofauti za wadau wa bandari ambayo itaongozwa na Daniel Silla toka Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ili kuchunguza na kubainisha kero zilizopo bandarini hapo na suluhisho zake.
Wajumbe wengine walioteuliwa ni sekta zao kwenye mabano ni Castrol Felician (TRA), Meshack Gideon (Dereva wa Ndani), Chacha Lukwi (Mshauri wa Madereva), Agness Mathias (KK Security), John Masasi (TICTS), William Kapera (TPA Usalama), Martin Paul (Evergreen Shipping Agent), Jones Jonathan (Wakala Usafirishaji) na Aloyce Gabriel (Wakala Uingizaji).
“Tarehe 03 mwezi Februari nataka ripoti ofisini kwangu ikiwa na uchunguzi mlioufanya ili kuiboresha bandari hii kwa kuwa nataka tuwe bandari ya mfano katika dunia hii” alisema Dk Mwakyembe.

CHANZO-GAZETI LA MWANANCHI

WATU NANE WAUAWAWA KATIKA VURUGU ZA MTWARA NA MOROGORO,NYUMBA ZA VIONGOZI ZACHOMWA MOTO

Wakazi wa mji mdogo wa Dumila Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro  wakiwakimbia askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU)  katika barabara ya Dodoma-Morogoro juzi.

HABARI KAMILI
WATU wanane wameuawa na wengine kumi na moja kujeruhiwa kutokana na vurugu zilizizotokea jana mkoani Mtwara na Itete wilayani Ulanga, mkoani Mororgoro.
Muuguzi wa zamu katika Hospitali ya Wilaya ya Masasi, Mkomaindo, Amima Simbo alithibitisha vifo vya watu saba waliofikishwa hospitalini hapo.
Kwa mujibu wa muuguzi huyo, maiti zilizopokelewa hospitalini hapo zilionekana zikiwa na matundu yanayodhaniwa kuwa ni ya risasi, baadhi yao kichwani, begani, viunoni na tumboni.
Aidha majeruhi waliofikishwa hospitalini hapo pia walikuwa na majeraha mbalimbali ikiwamo ya risari.
Habari zaidi zinaeleza kuwa vurugu hizo zilizuka baada ya kundi la waandamaji, wengi wakiwa vijana waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda waliokuwa wakipinga mwenzao kukamatwa na kutaka kuvamia Kituo cha Polisi ili kumwokoa.
Vurugu hizo ziliendelea kuutikisa Mkoa wa Mtwara kwa siku ya pili mfululizo na kuutikisa Mkoa wa Mtwara, baada ya vurugu nyingine kuibuka wilayani Masasi jana.
Habari zinasema mbali na vifo na majeruhi, nyumba za wabunge wawili wa wilaya hiyo zimechomwa moto, ambapo pia magari, trekta, Ofisi za CCM Wilaya na Ofisi ya Mkurugenzi wa Wilaya ziliharibiwa kwa kuchomwa moto.
Wabunge ambao nyumba zao zimemwa moto ni Mariam Kasembe wa Masasi Mjini na Anna Abdallah Mbunge wa Viti Maalumu wilayani humo.
Juzi vurugu hizo zilitokea katika Mikoa ya Morogoro kati ya wakulima na wafugaji na kusababisha kifo cha mtu mmoja wakati mkoani Mtwara wananchi  wa eneo la Chikongola waliizingira nyumba ya diwani wa Kata ya Mikindani, Mohamedi Chehako kwa madai ya kuwahifadhi wachawi ndani ya nyumba yake.
Katika vurugu hizo polisi walilazimika kutumia silaha yakiwamo mabomu ya machozi ili kupoza hali ya hewa, ambapo nyumba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia ilichomwa moto.
Akizungumza na Mtandao huu kuhusu vurugu hizo, Mbunge wa Masasi Mjini, Mariam Kasembe alisema kuwa nyumba yake iliyoko Masasi mjini imechomwa moto na kuteketea kabisa, huku mali zikiibwa na kwamba familia yake sasa haina makazi.
Aliongeza kwamba mbali na uharibifu, vurugu hizo zimesababisha pia mama yake mzazi kukimbia na mpaka sasa hajulikani alipo.
“Wamechoma trekta na gari lililokuwepo nyumbani kwangu, watoto wangu na mume wangu walipoona hali hiyo wakakimbia,” alisema Kasembe akieleza kuwa hawezi kuthibitisha chanzo cha vurugu hizo, lakini anahisi kuwa zinatokana na mgogoro wa gesi.
CHANZO-GAZETI LA MWANANCHI

Friday, January 25, 2013

SITA AJIPIGIA CHAPUO YA URAIS


.Asema anafaa  kuwa Rais

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta 
,”
HABARI KAMILI


WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amesema kwamba anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania na anafikiria kugombea 2015, iwapo dhamira yake itaridhika na mazingira na upepo wa kisiasa wa wakati huo.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na Mtandao huu Sitta alitaja mambo kadhaa aliyoeleza kuwa ni ishara ya kukubalika kwake, ikiwamo kuteuliwa na marais wote wanne; Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete katika nyadhifa mbalimbali ikiwamo ya uwaziri.
Kauli ya Sitta imekuja baada ya kuwapo kwa minong’ono ya baadhi ya wananchi kumtaja kuwa miongoni mwa watu wanaoweza kujitokeza kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
“Ni faraja kusikia watu wakinizungumzia kuwa ninazo sifa (za kuwa Rais). Nami ninaamini ninazo sifa. Wakati utakapofika nitajipima. Kama hali hii itaendelea, basi nitaona ni vizuri nigombee,” alisema Sitta ambaye aliwahi kuwa Spika wa Bunge.
Hata hivyo, alisema hana mkakati wowote sasa wa kuendesha harakati za kutafuta nafasi hiyo kwa udi na uvumba kama baadhi ya wengine (bila kuwataja), wanavyofanya... “Sina sababu za kuanza kutafuta support (kuungwa mkono) wala uundaji wa kamati za ushawishi kwa watu sasa,” alisema Sitta.
Badala yake alisema atasubiri hadi muda wa kuchukua fomu za kugombea utakapofika ndipo atakapojitathmini na kusema endapo atabaini kuwa Watanzania wengi wanamuunga mkono, atachukua uamuzi wa kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho.
Aitahadharisha CCM
Waziri huyo aliwahadharisha wanachama wa CCM kwamba wasipokuwa makini, wanaweza kuipoteza nafasi hiyo ya urais na kwenda kwa vyama vya upinzani.
Alionya kuwa iwapo watamteua mtu asiye mwadilifu, Watanzania hawatamchagua na badala yake watampa nafasi hiyo mgombea yeyote kutoka vyama vya upinzani.
Alisema Watanzania wengi wana werevu wa kutosha kujua watu ambao ni mafisadi na ambao wamekuwa wakitumia fedha zao chafu kwa ajili ya kutaka wakubalike mbele ya macho ya Watanzania. Alisema suala la uadilifu ni moja ya vigezo muhimu ambayo CCM wanapaswa kuvizingatia ili kupata ushindi wa kiti cha urais mwaka 2015.
“Ndiyo maana nilipokuwa mbele ya Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba niliweka wazi kwamba Tanzania tunahitaji kuwa na jopo la kuhoji viongozi na wananchi wawe na fursa ya kuwachambua,” alisema Sitta.
Alisema kinachohitajika Tanzania ni mfumo ambao utajenga mazingira ya kuwa na viongozi waadilifu katika ngazi zote.
Alisema hali hiyo itaepusha mfumo unaoonekana sasa wa viongozi kwenye ngazi mbalimbali kuishi kiujanjaujanja, kujinufaisha na kutojali athari kwa uchumi wa nchi na Watanzania kwa ujumla.
Alitoa mfano wa uzembe uliofanywa na viongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), ambao umesababisha Bandari ya Dar es Salaam kupoteza uaminifu kwa nchi mbalimbali zinazopakana na Tanzania.
Alisema uzembe huo umeifanya Bandari ya Dar es Salaam kuingiza Sh38 bilioni kwa mwezi tofauti na Mombasa ambayo inaingiza Sh300 bilioni.
CCM ni imara?
Akizungumzia miaka 36 ya kuzaliwa kwa CCM, mbunge huyo wa Urambo Mashariki alisema anaamini kwamba chama hicho kimefanya vizuri licha ya kuchafuliwa na watu wachache kutokana na tabia zao za ufisadi.
CHANZO-GAZETI LA MWANANCHI

Thursday, January 24, 2013

KIGAMBONI YAWA MJI UNAOJITEGEMEA

.yanyofolewa Temeke

(Picha na www.ippmedia.com)
 HABARI KAMILI
 
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya makazi, Prof Anna Tibaijuka akiuzungumza na waandishi wa habari juu ya serikali kuunda Wakala wa Uendelezaji wa mji wa Kigamboni jijini Dar es Salaam jana. 
 
Wengine ni Mkurugenzi wa Upimaji Ramani, Sellasie Mayunga (kushoto), Mkurugenzi Mipango Miji na Vijiji Albina Bura na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Uendelezaji wa mji wa Kigamboni, Vicent Shahidi.
Serikali imetangaza kuuondoa Mji wa Kigamboni kuwa chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Temeke na kuanzisha mamlaka ya upangaji wa mji huo ijulikanayo, kama Wakala wa Kusimamia Uendelezaji wa Mji Mpya wa Kigamboni (KDA).

KDA ambayo ilianzishwa na serikali kisheria Januari 18, mwaka huu, itasimamia uendelezaji wa mji huo unaotarajiwa kuwa wa kisasa.
      
Mji huo pia unatarajiwa kuwa kitovu cha kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika jiji la Dar es Salaam ili liweze kushindana na miji mingine duniani katika kuvutia uwekezaji, biashara na utalii na kukuza ajira, hasa kwa vijana.                                                                                                         Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, aliwaambia waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam jana, kuwa KDA itaongozwa na mkurugenzi mtendaji. Alisema mkurugenzi huyo atateuliwa pamoja na wakurugenzi sita watakaokuwa na wakuu wa idara.

Hata hivyo, alisema kwa sasa KDA inaongozwa na kaimu mkurugenzi mtendaji. Mbali na hilo, alisema KDA pia itasimamiwa na Bodi ya Ushauri pamoja na Baraza la Ushauri.

Alisema Baraza hilo litakuwa na wajumbe wanaowawakilisha wadau wote, hususan wabunge na madiwani wa eneo litakaloendelezwa na KDA.

Waziri Tibaijuka alisema KDA itakuwa na kazi ya kutafuta fedha za kutosha kwa ajili ya mradi, kupanga mji na kusimamia ujenzi wa mji kwa viwango vya kimataifa. Hata hivyo, alisema wananchi watashirikishwa kushauri.

Alisema fidia kwa wananchi ambao makazi yao yatatwaliwa kwa ajili ya kupisha uendelezaji wa mji itatolewa, lakini hawatahamishwa, badala yake watapewa makazi mapya katika mji huo mpya wa Kigamboni.

Hata hivyo, alisema ambaye atalipwa fidia hataruhusiwa kwenda kuishi katika makazi yaliyo nje ya mji mpya wa Kigamboni.

Alifafanua kuwa, atakayeruhusiwa ni yule atakayeonyesha hatimiliki ya kiwanja anachokwenda kujenga nje ya mji huo kwa ajili ya kuishi huko.

Waziri Tibaijuka alisema eneo litakalosimamiwa na KDA lina ukubwa wa hekta 50,934.
Alisema katika uendelezaji huo, kata zote za Kigamboni zimeunganishwa na kwamba, mji huo utaendelezwa na kuwa wa kisasa.

Waziri Tibaijuka alisema yeye ni miongoni mwa wataalamu duniani walioshiriki katika ujenzi wa mji wa Dubai.

Hivyo, akasema hataki kuona tena Watanzania wakifika Dubai waanze kuushangaa mji huo.
Alisema eneo la mji wa Kigamboni linahusisha Kata za Kigamboni, Tungi, Vijibweni, Mjimwema, Kibada, Somangila, Kisarawe II, Kimbiji na Pemba Mnazi.

Waziri Tibaijuka alisema katika kusimamia uendelezaji huo, KDA itaongozwa na mpango kabambe.

Alisema mpango huo ni pamoja na kuwa na mji uliopangwa kwa kiwango cha kimataifa utakaokuwa mfano wa kuigwa na miji mingine nchini.

Pia kupunguza ujenzi holela, kuongeza mapato ya serikali yanayotokana na shughuli za kiuchumi na kijamii, kama vile viwanda, hoteli, utalii, biashara, elimu, ofisi, afya na vituo vya michezo.

Vilevile, kupunguza msongamano wa magari na huduma za kiuchumi na kijamii katikati ya jiji la Dar es Salaam, kuongezeka kwa thamani ya ardhi katika maeneo ya mji kutokana na kuboreshwa kwa miundombinu ya barabara, maji na umeme itakayowezesha kukuza biashara, ujenzi wa majengo na viwanda.

Pia kuhamasisha uwekezaji ili kuongeza ajira, hasa kwa vijana na wananchi wengi wataweza kumiliki nyumba katika maeneo yaliyopangwa na kutumia nyumba zao kupata mikopo kwa ajili ya shughuli zao mbalimbali.

Alisema mji mpya wa Kigamboni utakuwa na watu takriban 400,000 kulinganisha na watu 80,000 waliopo sasa.

Waziri Tibaijuka alisema katika kutekeleza mpango huo, uwakilishi wa wananchi utakuwapo kama ambavyo umekuwapo katika mchakato wa ufanikishaji wake.

Hii ni hatua mpya na kubwa inachukuliwa na serikali katika kukabiliana na mradi wa Kigamboni ambao wananchi kadhaa wakiongozwa na Mbunge wao, Dk. Faustine Ndugulile, wanadai kuwa wananchi hawajashirikishwa katika mradi huo.

Tayari wananchi hao wameunda kamati ya kusimamia madai yao wakihofia kwamba huenda unalenga kuwapora maeneo yao na kuwapa wawekezaji wakubwa.

MBUNGE AZUNGUMZA
Ndugulie akizungumza na NIPASHE jana jioni, alisema anasikitishwa na hatua zinazozidi kuchukuliwa na serikali kwa eneo la Kigamboni bila kuwashirikisha wananchi.

“Kweli tunaanza mwaka mpya vibaya. Yaani hawa wameshindwa kuwashirikisha wananchi kwenye zile kata za awali nne sasa wameongeza zingine na eneo kubwa zaidi bila hata kuzungumza nao… huu  ni uvunjaji wa sheria, kwa nini lakini?” alihoji.

Mbunge huyo alisema ingawa dhana ya mradi huo ni nzuri, lakini kutokuwashirikisha wananchi ni uvunjaji wa sheria.
“Serikali inaendelea na ubabe na kuvunja sheria sijui ni kwa nini,” alisema.
 
CHANZO: NIPASHE

Tuesday, January 22, 2013

MKAPA KUTAKA SULUHU SUALA LA GESI KWAPOKEWA KWA HISIA TOFAUTI

Mkapa akoleza mjadala wa gesi

Rais Mstaafu Benjamin Mkapa 


HABARI KAMILI
WITO wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kutaka suluhu ya mgogoro wa gesi unaoendelea baina ya Serikali na wakazi wa mikoa ya kusini, umepokewa kwa hisia tofauti. Baadhi ya wasomi wamempongeza huku wakazi kadhaa wa Mtwara wakimpinga.

Juzi, baada ya mgogoro huo kuendelea kwa takriban mwezi mmoja sasa, Mkapa alizitaka pande hizo mbili kutafuta mwafaka akieleza kuwa linalowezekana leo, lisingoje kesho.

“Mtafaruku huu haufai kuachwa na kutishia usalama, mipango ya maendeleo siyo siri, mikakati na mbinu za utekelezaji wake siyo siri. Maelezo yake mazuri yanaweza kutolewa yakadhihirisha namna na kasi ambayo rasilimali zinawanufaisha wananchi wa eneo zilimo na taifa zima,” alisema Mkapa katika taarifa yake.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana alisema jana kuwa kauli ya Mkapa ni nzuri, huku akisisitiza kuwa katika suala hilo, lazima utaifa uwekwe mbele.
“Hata wakati wa ujenzi wa Barabara ya Mtwara, wapo waliosema kuwa mikoa ya kusini inatengwa, kauli hizi zilikuwapo tangu zamani, kikubwa ni suala hili kuchukuliwa kitaifa zaidi,” alisema Dk Bana.

Wazee watafuta suluhu Dar
Wazee wa Mtwara Mikindani wako Dar es Salaam kusaka suluhu ya mgogoro huo, baada ya kusema kwamba wamebaini kuwa kutakuwa na uvunjifu wa amani kama suala hilo litaachwa liendelee.

Wakizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, wazee hao walisema suala hilo linaleta hofu kubwa kwa taifa hivyo linapaswa kupatiwa ufumbuzi wa haraka.
Katibu wa wazee hao, Selemani Mademu alisema wananchi wa Mtwara wako tayari kufa kuliko kuona wakidharauliwa katika suala hilo.

Mademu alisema: “Wananchi wa Mtwara wanaamini kuwa kituo cha kuchakata gesi asilia kama kitajengwa Mtwara kitatoa fursa kubwa ya kushawishi wawekezaji ambao watajenga viwanda vitakavyotumia malighafi ya gesi asilia na hivyo kuchochea maendeleo ya Mtwara kwa jumla,” alisema na kuongeza kuwa kama Serikali inaamini kwamba wazo lake la kuisafirisha hadi Dar es Salaam ni jema na lenye manufaa kwa wananchi wa Mtwara, ingejikita katika kutoa elimu badala ya kukaa kimya na kuendelea na kile inachoamini.

“Wanamtwara hatupendi kuendelea kuelezwa kwamba tutanufaika na gesi iliyogunduliwa kwa kuahidiwa viwanda kama ambavyo imekuwa desturi ya Serikali yetu. Tunahitaji vitendo vitawale badala ya ahadi ambazo hazitekelezeki. Kwa mfano barabara, umeme, kuimarishwa kwa bandari, mikopo kwa ajili ya ujasiriamali, viwanda vidogo vya kubangua korosho n.k.” alisema.

Wengine wapinga
Mwenyekiti wa Umoja wa Maendeleo Mikoa ya Kusini (UMMK), Said Mannoro (72) alimshutumu Mkapa akidai kuwa ndiye chanzo cha gesi ya Songosongo kupelekwa Dar es Salaam.

Mzee Mannoro ambaye alifika katika ofisi za gazeti hili, Tabata Relini, Dar es Salaam jana alisema Mkapa anatakiwa kueleza faida walizopata wananchi wa Lindi baada ya gesi ya Songosongo inayozalishwa mkoani humo, kupelekwa Dar es Salaam.

Mbali na mzee huyo, baadhi ya viongozi wa dini na vyama vya siasa nao wamempinga Mkapa wakisema kuwa ushauri wake umeegemea upande mmoja na kwamba alipaswa kumshauri Rais Jakaya Kikwete.

Askofu Mteule wa Kanisa la KKKT Dayosisi Mpya ya Kusini Mashariki, Mchungaji Lucas Mbedule alisema Mkapa, amechelewa kutoa ushauri wake na kwamba kwa hali ya sasa alipaswa kumshauri Rais Kikwete akubaliane na matakwa ya wananchi.
CHANZO-GAZETI LA MWANANCHI

Friday, January 18, 2013

MAKALA YA MGANGA WA JADI BINTI NDEMBO NA UCHAWI


Mganga wa Jadi wa Namtumbo Songea Frola Ndembo Maarufu kwa jina la Binti Ndembo.

Ndugu Wasomaji wa Mtandao huu tunawaletea  Makala ya Binti Ndembo na Uchawi na Mchambuzi   wako wa masuala ya Uchawi Mwanahabari Adam Nindi.

Fuatana naye

Kwa habari za kina nilikuwa nikiifahamisha Jamii kwa kitu kinachoitwa uchawi ambacho ndicho changamoto kwa watu wanaoishi pembezoni.
Watu walio wengi huingiwa na hofu kufanya Maendeleo kwa kile kinachoitwa woga wa kuuwawa au kulogwa. Kwani sumu ya kitu uchawi ni kuona maendeleo ya mtu mmoja mmoja.

                 Mganga wa jadi bint Frola Ndembo
Nikiwa katika kambi ya Mganga mashuhuri wa Nyanda za juu Kusini Mama Binti Flora Ndembo nimeweza kupata siri kubwa kuhusu uchawi. Wachawi wenyewe wamesema wamejiingiza katika uchawi baada ya kuona Jamii ikiwatenga, wale ambao ambao hawana uchumi wa kutosha ndio wanaunda umoja wa kuwatesa wenzao.

Mchawi mkuu wa wachawi wote ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali Serikalinina hatimaye kuchaguliwa kuwa katibu wawachawi mkoa wa Ruvuma  amesema yeye alijiunga na uchawi kwa ajili ya kutaka kujikinga na watu wabaya  lakini mara baada ya kustaafu alipendekezwa kuwa Katibu Mkuu wa wachawi Mkoa wa Ruvuma.
Lakini yeye mwenyewe amesema ameamua kujitoa baada ya wachawi wenzie kumuua mototo wake ambaye alifikia ngazi ya kuwa Askofu; hapo ndipo alipoona kuwa uchawi hauna maana.
Nikiwa mchambuzi wa habari za ushirikina  niliamua kumuuliza mzee kuwa mootto wake ambaye alikuwa mtu wa Mungu aliwezaje kuuwawa wakati yeye ndiye aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wachawi. Alijibu hakuna mtu anayeweza kuuwa katika ukoo kama ndugu hajaidhinisha na sheria hiyo hufuatwa kwa makini ukikiuka taratibu unauwawa mwenyewe “ndivyo ilivyonikuta kwa mototo wangu

Nikiwa katika Kambi hiyo ya Binti Ndembo nilikutana na Mwenyekiti wa wachawi katika maeneo ya Mwambao wa ziwa nyasa. Yeye anasema alijitenga na Jamii na alikuwa akiishi mashambani ambako ndiko kulikuwa Makao Makuu ya Mikutano ya wachawi wote.
Yeye anasema alijiunga na uchawi baada ya kaka yake kuweka rehani mwili wake baada
Nikiwa katika Kambi hiyo ya Binti Ndembo nilikutana na Mwenyekiti wa wachawi katika maeneo ya Mwambao wa ziwa nyasa. Yeye anasema alijitenga na Jamii na alikuwa akiishi mashambani ambako ndiko kulikuwa Makao Makuu ya Mikutano ya wachawi wote.
Yeye anasema alijiunga na uchawi baada ya kaka yake kuweka rehani mwili wake baada
wa kuuwawa au kulogwa. Kwani sumu ya kitu uchawi ni kuona maendeleo ya mtu mmoja mmoja.
Nikiwa bado katika Kambi hiyo ya Binti Ndembo, nilitiwa na fadhaha baada ya kumuona Binti mwenye umri wa miaka 10 aliyepewa uchawi na Mama yake na kuweza kupewa mboga ya akiba ambacho ni kidonda kilicho ubavuni ambacho yeye alikiri kuwa akikosa mboga hutumia kwa kuchovya kwenye kidondaMaskini Binti huyo katika maisha yake hadi kufikia miaka hiyo 10 alikuwa akichukia shule kama nini lakini baada ya kufika kwa Binti Ndembo ameacha uchawi na kuomba akaendelee na Masomo

Kamanda wa Polisi aliye hamia Iringa Michael Kamuhanda kushotona Kamanda Mpya Mkoa wa Ruvuma Deusdedit Kaizilege Nsimeki
 Ndugu yangu nikiwa katika kambi hiyo na Binti Ndembo nimeona mambo mengi cha kufurahisha mganga huyo hana uchochezi. Yeye amekuwa akipatanisha ndugu hao na kuwa Jamii moja. Nikiwa Kambini hapo nimeshuhudia Viongozi wa ngazi za juu akiwemo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma akitoa elimu Shirikishi kwa kutaka Jamii iachane na Mambo ya Ushirikina.
Mganga huyo mashuhuri mbali ya kutibu watu wenye asili ya Ushirikina lakini hata hivyo ameshaweza kukamata Majambazi Sugu, na wao kusalimisha silaha zao na kuachana na Ujambazi.
Jambo la kuingilia Masuala ya Ujambazi, Mganga huyo mashuhuri amepata misukosuko kwa kuwahi kupigwa risasi mbili na kukimbizwa Hospitali ambako alitolewa.
Amewahi kufungwa Kamba na kutupwa msituni na kuambiwa aachane na masuala ya kufuata Majambazi lakini uganga wake uliweza kumwokoa.
Pia kwa Mara ya Kwanza Mganga huyo aliweza kubainisha ndoa iliyofungwa kati ya Mama na Mtoto wake wa kuzaa mwenyewe. Hatimaye aliweza kuibainisha Ndoa hiyo hadharani.
   Ndugu zangu wasomaji, Shabaha yangu ni kutaka kuendelea kupata mawazo kutoka kwenu, kitu kikubwa ambacho kinasababisha Maendeleo kuto chukua Kasi ni Kushiriki katika Mambo ya Ushirikina.   Sasa hapa tumeona watu walio wengi wakiacha Uchawi na kutangaza Hadharani.

HALI YA DCI MANUMBA BADO MBAYA,BADO YUKO ICU


Rais Jakaya Kikwete akiongozana na Inspekta Jenerali wa Polisi katika Hospitali ya Aga Khan ya jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumlaki Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI)  Kamishna Robert Manumba aliyelazwa hospitalini hapo. 
e

 FULL STORY

HALI ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Jeshi la Polisi (DCI), Robert Manumba bado ni mbaya na jana Rais Jakaya Kikwete alikwenda tena ikiwa ni mara ya pili mfululizo katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam alikolazwa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), kumjulia hali.

Mbali na Rais Kikwete, viongozi wengine waliofika hospitalini hapo kumjulia hali DCI Manumba ni Mke wa Rais, Salma, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP, Said Mwema na Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni. Pia walikuwapo ndugu, jamaa na marafiki ambao walikusanyika hospitalini hapo takriban siku nzima jana wakifuatilia afya yake.

Rais Kikwete alifika hospitalini hapo jana saa 11:15 na alitumia takriban dakika 10 tu kwani alitoka saa 11:26 huku akionekana mnyonge na alielekea kwenye gari lake na kuagana na IGP Mwema na Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan, Dk Jaffer Dharsee kisha kuondoka.

Juzi, Rais Kikwete alikwenda hospitalini hapo mara baada ya kumsindikiza Uwanja wa Ndege mgeni wake Rais wa Benin,Thomas Boni Yayi aliyekuwa nchini kwa ziara ya siku moja.
Jana, Mke wa Rais alikuwa wa kwanza kufika hopitalini hapo saa 10:20 na aliondoka saa 10:45 muda mfupi kabla ya Rais Kikwete kufika.

Habari zilizopatikana jana zilieleza kwamba kutokana na afya yake kuwa mbaya, wageni wengi wakiwamo viongozi waandamizi, walizuiwa kuingia kumwona.
Uongozi wa Aga Khan watoa tamko
Jana mchana, uongozi Aga Khan ulitoa taarifa rasmi kuzungumzia afya ya kiongozi huyo wa Polisi huku ukieleza kuwa kimsingi siyo nzuri na bado anahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari.

“Uongozi wa Hospitali ya Aga Khan ungependa kuujulisha umma kwamba Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini, DCI Robert Manumba bado yupo hospitalini Aga Khan ambako anaendelea kupatiwa matibabu. Hali yake bado inahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Juzi, Dk Dharsee alisema Manumba alifikishwa katika hospitali hiyo akisumbuliwa na malaria huku hali yake ikiwa mbaya na hajitambui.

Msemaji wa familia atoa mafumbo
Akizungumza na waandishi wa habari hospitalini hapo jana, msemaji wa familia ya DCI Manumba, James Kilaba alisema: “Maisha ndivyo yalivyo, huwezi kuzua ugonjwa na huwezi kubadili uhalisia wa mambo. Sisi kama familia, tunaamini Mungu yuko na ndugu yetu na ndiye atatenda yake na naomba Watanzania wamuombee.”

Hata hivyo, alikataa kuzungumzia ugonjwa wake zaidi ya kusema kuwa alipelekwa Jumanne iliyopita hospitalini hapo kwa ajili ya vipimo zaidi.
CHANZO-GAZETI LA MWANANCHI

WAJAWAZITO WADAI KUNYANYASWA MALAWI KUTOKANA NA MGOGORO WA ZIWA NYASA

Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Malawi Joyce Banda, wakitabasamu huku wakipeana mikono mara baada ya mazungumzo mjini Maputo
WAKATI mzozo wa mpaka wa Ziwa Nyassa unaoendelea kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali na Malawi haujapatiwa ufumbuzi, mamia ya Wajawazito kutoka Tanzania kuelekea nchini Malawi kupata huduma ya Afya wamedai kunyanyaswa na baadhi ya watoa huduma katika Hospitali nchii humo.
Wakizungumza na Mtandao huu kwa nyakati tofauti huku wakiomba majina yao kutotajwa mtandaoni kwa madai kwamba bado wanategemea kupata huduma hiyo nchini humo, wamesema kwamba tangu mzozo huo ulipoanza wamekuwa wakipata huduma hiyo kwa shida tofauti ya siku za nyuma,
"Tangu mzozo wa mpaka wa Ziwa Nyassa tumekuwa na wakati mgumu wa kupata huduma ya afya  kwa sababu baadhi wataalaam wa afya nchini humo hawataki kutuhudumia kwa wakati kwa madai kwamba hivi sasa nchi zetu hazina mahusiano mazuri kutokana na mzozo huo"aliema mama mjamzito ambaye ni mkazi ya kijiji cha Ikumbilo.
Ramani ya TanzaniaAkizungumzia sababu za wao kwenda kutafuta huduma ya afya nchini humo alidai kwamba ni kukiukwa kwa sera ya Afya ya mwaka 2007 inayosema kwamba wajawazito nchini Tanzania watapewa huduma za afya bure.
"Sera hiyo imekiukwa katika Hospitali za Wilayani Ileje Mkoani Mbeya,ndiyo maana baadhi ya wajawazito wilayani Ileje wanaacha Zahanati, vituo vya Afya na Hospitali Wilayani humo na kuvuka mpaka hadi nchi jirani ya Malawi kufuata huduma bora, tumekuwa tukivuka mpaka huu kwa miaka mingi,mfano mimi mwenyewe ninawatoto watano hivi sasa na wote nimewaza nchini Malawi"alifafanua mjazito mwingine.
Wajawazito hao wanatoka kata za Bupigu, Itumba na Isongole na wnakwenda nchini Malawi kwa wingi ili waweze kujifungulia huko na kupata huduma nyingine za afya.
Kutoka Isongole hadi Hospitali maarufu ya Chitipa nchini Malawi ni umbali wa kilometa 45, wakati umbali wa kwenda Hospitali ya Serikali ya Ileje ni kilomita tatu tu. Mwanamke moja mkazi wa kijiji cha Ikumbilo, kata ya Chitete wilayani Ileje, aliyejitambulisha kuwa anaishi na virusi vya ukimwi (VVU) anasema aliwahi kujifungulia Hospitali ya Chitipa na mpaka sasa anapata matibabu yake huko. Wilaya ya Ileje ina Hospitali kubwa mbili – Hospitali ya Serikali mjini Ileje na ile ya Misheni ya Isoko.ambapo ndizo Hospitali ambazo zinategemewa kwa huduma ya uzazi.
CHANZO-HABARI MPYA.COM

Tuesday, January 15, 2013

VIJANA MSISUKUMWE KATIKA MAKUNDI YA KUVURUGA AMANI-KIGWENEMBE

 Mjumbe wa Baraza kuu la V ijana wa CCM  Taifa  akizungumza kwa hisia kali katika moja ya mikutano yake.
 Alfan Kigwenembe akizungumza na Vijana katika moja ya Mkikutano yake.
 
VIJANA MSISUKUMWE KATIKA MAKUNDI YA KUVURUGA AMANI-KIGWENEMBE
Na Joseph Mwambije,
Songea
VIJANA  wametakiwa kutosukumwa katika makundi ya kuvuruga amani,kutumika kisiasa na kuandamana bila sababu za msingi na matokeo yake wao ndio wanaoathirika katika vurugu za kisiasa na maandamano na kuziacha familia zao zikiahangaika.
Wito huo ulitolewa juzi na mjumbe wa Baraza kuu la vijana wa CCM(UVCCM)Alfan Kigwenembe  wakati akizungumza na vijana kwenye mkutano wa hadhara katika Kata ya Msamala mjini Songea mambo mbalimbali yanayowahusu Vijana.
Mwanasiasa huyo kijana alikuwa akizungumza na Vijana wote wa Manispaa ya Songea bila kujali itikadi zao za kisiasa kwa kuwa wao ndio rasilimali  ya Taifa na wamekuwa wakitumika vibaya na Wanasiasa kwa maslahi yao.
Alibainisha kuwa katika maandamano zinapotokea fujo vijana wanaathirika kwa kupata ulemavu wa maisha na wakati mwingine kupoteza maisha na kuziacha familia zao zikihangaika huku Viongozi wa  Siasa waliowasukuma kuandamana wakishindwa kuwasaidia na kusaidia familia zao baada ya wao kupoteza maisha.
‘Vijana lazima mtambue kuwa nyinyi ni rasilimali ya Taifa hivyo hampawi kushiriki katika fujo na kuvuruga amani ya Nchi yetu na kuandamana katika maandamano yasiyokuwa ya msingi na badala yake mjiunge katika Vikundi vya ujasiriamali ili mjiletee maendeleo’alisema Mwanasiasa huyo.
Aliwataka vijana kufanya kazi kwa bidii ili kujileteaaendeleo kwa kuwa maisha bora hayaletwi kwa kucheza bao na Pool na badala yake yanaletwa kwa kufanya kazi kwa bidii na kuongeza kuwa miradi mbalimbali ya madini Mkoani Ruvuma ukiwemo wa Urenium utaongeza ajira kwa Vijana.


Alfan Kigwenembe

KUPINGA GESI KUSAFIRISHWA NI KUPINGANA NA BABA WA TAIFA-NCHIMBI


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana(UVCCM) Mkoa wa Ruvuma,Alex Nchimbi akizungumza wakati akifungua Baraza la UVCCM  Mkoa wa Ruvuma.Kulia ni Katibu wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Ruvuma,Mwajuma Rashid.


KUPINGA GESI KUSAFIRISHWA NI KUPINGANA NA BABA WA TAIFA-NCHIMBI

Na Joseph Mwambije
Songea

MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa CCM(UVCCM) Mkoa wa Ruvuma Bw. Alex Nchimbi  amesema kuwa kupinga gesi kusafirishwa kwenda Daressalaam ni kupingana na Baba  wa Taifa Hayati Julius Nyerere  aliyetaka kuwepo na mgawanyo sawa kwa rasilimali za Taifa kwa Mikoa yote Nchini.
Alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua  Barazaza la Vijana wa Chama hicho lililofanyika hivi karibuni mjini Songea na kuwataka Vijana wa Chama hicho kuwa makini wanapozijibia hoja za Kitaifa si kukurupuka kama hiyo ya gesi.
Alisema kuwa Baba wa Taifa  aliweka mgawanyo sawa wa rasilimali za Taifa na kuondoa ubaguzi wa kidini na Kikabila huku akiitambulisha lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya Taifa.
‘Tukisema rasilimali zinufaishe Mkoa husika pekee je Mikoa isiyokuwa na kitu itafanyaje,kwa sisi Mkoa wa Ruvuma mahindi yetu yamekuwa yakilisha Tanzania yote na Nchi nyingine za jirani’alisema.
Aliwataka Vijana hao kushirikiana na Jamii klatika masula ya kijamii pamoja nma elimu katika Shule za Sekondari na Shule za Msingi ambako alidai kuwa huko Umoja huo umekuwa ukipwaya wakati Vyama vya upinzani vimejikita kwa kiwango kikubwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Bw. Joseph Mkirikiti ambaye alikuwepo kwenye Baraza hilo  aliwataka Vijana kushirikiana katika kuijenga Jumuiya yao ya UVCCM na Chama chao kwa ujumla huku wakiwaunga mkono wanaokijenga Chama hicho badala ya kuwapinga.
Alimpongeza mjumbe wa Baraza kuu la Umoja wa Vijana Taifa Bw. Alfan Kigwenembe kwa kazi nzuri ya kufanya mikutano na kuongea na vijana mbalimbali wa Chama hicho na ambao si wa Chama hicho huku akiyazungumzia masuala mbalimbali ya msingi na kuyatolea ufafanuzi.