Tuesday, October 30, 2012

Purukushani migodini nchini A. Kusini

Wafanyakazi wa migodi wanaogoma

Makabiliano makali yamezuka kati ya Polisi na wachimba migodi katika mgodi wa madini ya Platinum wanaogoma Kaskazini Magharibi mwa Johannesburg.
Polisi waliwafyatulia risasi za mipira na kuwarushia waandamanaji gesi ya kutoa machozi katika makabiliano hayo ambapo wachimba madini hao wanataka nyongeza ya mishahara.
Kampuni ya Anglo-American Platinum imekubali kuwarudisha kazini wachimba madini elfu kumi na mbili waliofutwa kazi na kuwalipa malimbikizo ya mishahara, suala lililokataliwa mbali na wachimba madini hao.
Msururu wa migomo ya wachimba migodi na madini imeendelea kukumba Afrika Kusini katika miezi ya hivi karibuni na kuathiri pakubwa uchumi wa nchi hiyo.
CHANZO-BBC

No comments:

Post a Comment