Tuesday, November 13, 2012

BENKI YA WANANCHI NJOMBE YAKOPESHA SHILINGI BILIONI 4.6

 Jengo la Benki ya Wananchi Njombe
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki y Wananchi Njombe Bw. Michael Ngwira


BENKI YA WANANCHI NJOMBE YAKOPESHA SHILINGI BILIONI  4.6
 .Wananchi wainua maisha yao kiuchumi
.yatoa mikopo ya kilimo
Na Joseph Mwambije,
Njombe                             
BENKI ya Wananchi Njombe(NJOCOBA) Wilayani Njombe katika Mkoa mpya wa Njombe  imetoa mikopo ya shilingi Bilioni 4.6 toka ianzishwe Septemba  2010 kwa wananchi zaidi ya 3000 wa kada mbalimbali na kuyainua maisha yao kiuchumi.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa  Benki hiyo Bw. Michael Ngwira wakati akizngumza na Mtandao huu Ofisini kwake mjini Njombe  namna Benki hiyo inavyowawezesha wananchi kiuchumi na kusaidia katika kupambana na Umaskini.
Anasema kuwa walianza kukopesha Oktoba 2010  kwa watu,SACCOS na Vikundi mbalimbali vya maendeleo   na kwamba wamekuwa wakitoa elimu namna ya kuitumia sekta ya kifedha.
Mkurugenzi huyo anabainisha kuwa katika Kitengo chao cha mikopo wameanza kukopesha mikopo ya kilimo vijijini ambayo imeanza Septemba mwaka huu na tayari wameshakopesha shilingi milioni.
‘Katika mikopo ya  kilimo riba yetu imekuwa ndogo sana kuliko Benki nyingi ambapo tumekuwa tukitoa riba ya asilimia 8 na kufanya mikopo yetu ichangamkiwe na watu wengi na kwa sasa tuna maombi ya mikopo ya shilingi Bilioni 6,’anasema Mkurugenzi huyo.
Anasema kuwa Benki hiyo imekubalika  sana vijijini ambako wananchi wengi wanahitaji huduma zao na kubainisha kuwa wao wanalenga kuwasaidia wananchi ndio maana wanapeleka huduma huko ambako Taasisi za Kibenki ni chache.

No comments:

Post a Comment