Tuesday, November 20, 2012

MVUA NJOMBE ZASABABISHA HASARA YA SHILINGI MILIONI 241


MVUA NJOMBE ZASABABISHA HASARA YA SHILINGI MILIONI 241
Na Joseph Mwambije,
Njombe
HALMASHAURI ya Mji wa Njombe Mkoani Njombe imefanya tathmini ya  mvua zilizonyesha hivi  karibuni na kuharibu nyumba 178 na kubainisha kuwa maafa hayo yamegharimu shilingi milioni 241.

Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Njombe  Bw. George Mkindo anasema mvua hizo zilizonyesha hivi karibuni na kuambatana na upepo mkali zImesababisha Kaya zaidi ya 100 kukosa mahala pa kuishi na kuharibu mashamba na nafaka majumbani.

Anasema kuwa Uongozi wa Halmashauri hiyo umefanya tahmini na kubainisha hasara iliyotokana na mvua hizo kuwa ni shilingi milioni 241 huku akiomba Wasamaria wema kuwasaidia wananchi waliokumbwa na maafa hayo.

‘Mvua zile licha ya kuharibu mazao mashambani na nyumba lakini pia zimeharibu miti na mali mbalimbali na kuwasababishia wananchi kukosa mahali pa kuishi’anasema Mkurugenzi huyo.

Anasema kuwa mvua hizo zilileta madhara zaidi  katika vijiji vya Kibena ambako nyumba 91 ziliharibiwa na mvua,katika kijiji cha Nundu nyumba 35 na maeneo ya  Hospitali ya Kibena numba 15.

Anataja maeneo mengine kuwa ni katika kijiji cha Ngalanga ambako nyumba saba zimeharibiwa,kijiji cha  Hagafilo Nyumba mbili na katika kijiji cha  Peluhanda nyumba moja.

Amewashukuru wananchi waliotoa ushirikiano katika kuwasaidia wenzao waliokumbwa na maafa na kuwataka kuendelea na moyo huo wa kusaidiana na kubanisha kuwa mvua hizo hazikuleta madhara katika maeneo ya mjini.

No comments:

Post a Comment