Sunday, November 25, 2012

RAIS PAUL KAGAME AUNGA MKONO MPANGO WA KUMALIZA MAPIGANO CONGO

 Rais Paul Kagame wa Rwanda ametangaza kuwa anaunga mkono mpango uliopendekezwa na viongozi wa Maziwa Makuu, ili kumaliza mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.

Rais Paul Kagame
Rais Kagame aliisihi serikali ya Congo na wapiganaji wa M-23 kutekeleza mapendekezo hayo, ambayo piya yanataka wapiganaji hao waondoke katika mji wa Goma.
Rwanda inakanusha tuhuma za muda mrefu kwamba inawasaidia wapiganaji hao upande wa pili wa mpaka wa Rwanda.
Rais Kagame hakuhudhuria mkutano wa viongozi uliofanywa Kampala, Uganda, Jumamosi ambapo mpango huo ulikubaliwa.
CHANZO-BBC

No comments:

Post a Comment