Tuesday, January 15, 2013

RC RUVUMA AWAASA WANANCHI KUSHIRIKIANA NA KIKOSI CHA ZIMAMOTO KWENYE MAJANGA YA MOTO

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabiti Mwambungu akizungumza kwenye uzinduzi huo.
  
Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Ruvuma Baraza Mvano akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi  RC  Mwambungu.

RC RUVUMA AWAASA  WANANCHI KUSHIRIKIANA NA ZIMAMOTO KWENYE MAJANGA YA MOTO
Na Joseph Mwambije
Songea
MKUU wa Mko wa Ruvuma  Bw. Said Mwambungu amewataka Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kushirikiana na Jeshi  la Zimamoto katika uzimaji wa moto yanapotokea majanga ya moto badala ya kuwatupia mawe na kuwafanyia fujo Askari wa Kikosi cha zimamoto.

Alitoa wito huo jana wakati akizindua Zoezi la kuzima moto lililofanywa na Kikosi cha Zimamoto Mkoa wa Ruvuma na kufanyika  kwenye Viwanja vya Bustani za Manispaa ya Songea na kubainisha kuwa katika majanga ya moto mtu wa kwanza katika kuzima moto ni mwananchi mwenyewe.

‘Muwe  mnatoa taarifa mapema kwa Kikosi cha Zimamoto  badala ya kuchelewa kutoa taarifa na Askari wa Zimamoto wana pochelewa  mnawalaumu na kuwafanyia fujo wakati nyie wenyewe mmechelewa kutoa taarifa’alisema na kuongeza

Tatizo lenu mmekuwa mkijaribu kuzima kwanza wenyewe moto  pindi yatokeapo majanga ya moto mkishindwa ndio mnawaita Askari wa Zimamoto wakati moto umeshaunguza kila kitu hivyo ni vema mkabadilika na kutoa ushirikiano kwa  Kikosi cha Zimamoto.

Mwambungu aliongoza zoezi  la kuzima moto katika Operesheni maalumu ya kuzima moto iliyoandaliwa na Kikosi cha Zimamoto huku  Mtandao huu Cresensia Kapinga akiongoza kuzima moto kwa niaba ya Wanahabari wa Mkoa wa Ruvuma.

Kwa upande wake Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto Bw. Baraza Mvano alisema kuwa majukumu ya Jeshi la Zimamoto ni kuzima moto  wenye madjhara pale unapotokea,kuokoa maisha ya watu  na mali zake,kufanya ukaguzi wa Kinga na tahadhari ya moto na kutoa mafunzo ya kinga na tahadhari.

Baadhi ya Wananchi wakiongozwa na Amoni Mtega na Samweli Mapunda wamesema kuwa mafunzo na elimu iliyotolewa na Jeshi la Zimamoto katika Zoezi hilo imewasadia kuelewa Jeshi hilo linavyofanya kazi na hivyo watatoa ushirikiano kwa Kikosi hicho pindi majanga ya moto yanapojitokeza.
 
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabiti Mwambungu akizima moto
 Mashauri wa Mgambo mkoa wa Ruvuma Kanali Fula akizima moto
 Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Majira Mkoa wa Ruvuma Bi. Cresensia Kapinga akizima Moto
 Askari wazima moto wakizima moto

No comments:

Post a Comment