Sunday, July 8, 2012

JESHI LA POLISI RUVUMA LAKIRI KUMSHIKILIA MFANYABIASHARA MAARUFU MKOANI HUMO KWA TUHUMA ZA UJAMBAZI

Mwandishi wetu,
Songea

Jeshi la  Polisi Mkoani Ruvuma  limethibitisha kumshikilia na kumuhoji Mfanyabiashara  maarufu Mkoani humo wa vifaa vya maofisini(Stationaries) Shukuru Changwa kwa tuhuma za ujambazi.

Akizungumza na Waandishi wa habari Ofisini kwake juzi Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma,Deusdedit Nsemeki alisema  ni kweli walimshikilia na kumuhoji Mfanyabiashara huyo kwa  siku kadhaa wakimhusisha na  matukio ya ujambazi huku ndugu zake na wafanyabiashara wenzake wakihaha kumtoa korokoroni alikokuwa akishikiliwa.

Tukio hilo la kuhusishwa kwa Mfanyabiashara huyo na matukio ya ujambazi  limegusa hisia za watu wengi  kwa vile ni muumini wa dhehebu moja la kilokole huku Kamanda Nsemeki akisisitiza kuwa Mfanyabiashara maarufu si tiketi ya kufanya ujambazi.

“Unajua nilishangazwa na  tukio la  la kushambuliwa kwa risasi kwa Mfanyakazi wa  Kampuni ya Mohamed Enterprises majira ya saa mbili asubuhi na kuporwa nyaraka ambazo Wavamizi walizidhania kuwa ni fedha’a;isema Kamanda huyo na kuongeza

Na tulipofuatilia tukagundua nyuma ya pazia kuna Wafanyabiashara wakubwa wa mjini hapa wanahusika,hivyo acha wazungumze maneno yao mitaani kwamba tumewaonea na kuwadhalilisha lakini bado tunaendelea na uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani.

Alisema liko genge la Wafanyabiashara linaliojihusisha na ujambazi na ndio maana ujambazi umekuwa ukifanyika hata majira ya mchana   ambapo anasema yeye hawamtishi na wakibainika watachukuliwa hatua bila kujali pesa zao.

Kamanda huyo kijana ambaye  pia  Mkoa wa Ruvuma ni wa kwaza  kufanyia kazi akiwa Kamanda wa Mkoa alisema Jeshi lake limejipanga vyema kuhakikisha amani iliyopo inadumishwa hivyo mtu yoyote anayejaribu kuvunja sheria atashughulikiwa bila kujali nafasi yake katika jamii.

Alisema ulinzi katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji utaimarishwa ili kuzuia kuingia kwa silaha toka Nchini humo lakini pia aliwaomba Wananchi na Waandishi wa habari Mkoani humo kumpa ushirikiano katika kuwafichua wahalifu.

Katika hatua nyingine wananchi Mkoani humo wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Kamanda huyo  katika kupambana na uhalifu ambapo hivi karibuni Jeshi lake Mkoani humo lilifanya Operesheni maalumu ya kuwasaka wahalifu na kufanikiwa kukamata silaha,bangi,pombe ya moshi na kukamata mali za wizi.

Tukio hilo linakuja baada ya matukio ya hivi karibuni ya Mkandarasi mmoja kumfyatulia risasi mbili Askari Polisi na kumjeruhi kwenye mapaja yote mawili na jingine la Mfanyabiashara mmoja wa Kitukio cha Mafuta cha Kisumapai na Mkurugenzi wa Kituo hicho  kuporwa milioni 30 na Majambazi.

Katika tukio laKisumapai kuporwa milioni 30 lilikuwa kama Sinema za mapigano hivi kwani Wanyang’anyi walimvamia majira ya saa 3 usiku wakati akirejea nyumbani  akiwa kwenye gari lake ambapo walipiga risasi kwenye tari la gari lake na kumuamuru awape mfuko wenye pesa.

Wakati wakimuamrisha kutoa pesa motto wake wa kike ambaye alikuwa naye kwenye gari aliwarushia mkoba wake wakasema si huo awape mfuko mweupe ndio wenye opesa.
Mwisho

No comments:

Post a Comment