Monday, August 27, 2012

Apple yaipiku Samsung mahakamani

Apple yaipiku Samsung mahakamani

Na Mashirika Ya habari

Jopo la mahakama moja ya Marekani limeamua kuwa kampuni kubwa ya teknolojia ya Korea Kusini, Samsung, iliiga baadhi ya ufundi mpya wa kampuni ya Marekani ya Apple kuunda simu zake wenyewe za kisasa za smartphone na kumputa ndogo - tablet.
Simu za Apple na Samsung
Baada ya kesi iliyoendelea kwa mwaka mzima, ambayo ilichunguza mashtaka kama 700 ya aina ya ufundi ulioigwa, mahakama ya California yaliiamrisha Samsung iilipe Apple fidia ya dola zaidi ya bilioni moja.
Samsung imelalamika kuwa Apple inajaribu kuhodhi soko zima la smartphone, na imesema itakata rufaa.
Zaidi ya nusu ya simu za smartphone zinazouzwa duniani ni ama za Apple au Samsung, na kampuni hizo mbili zinashtakiana katika mahakama ya nchi mbali mbali duniani.

No comments:

Post a Comment