Monday, November 12, 2012

WANANCHI NA WAWEKEZAJI WATAKIWA KUCHANGAMKIA VIWANJA NJOMBE

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmaashauri ya Mji wa Njombe Bw. George Mkindo

.HALMASHAURI YA MJI WA NJOMBE IMEPIMA VIWANJA 700

 .VIWANJA 206 VIMESHANUNULIWA
.VIMEBAKI VIWANJA  494
Na  Joseph  Mwambije,
Njombe
HALMASHAURI ya mji wa Njombe Mkoani Njombe imepima Viwanja  700 katika maeneo ya Mjimwema Mkoani humo na tayari imeshauza  viwanja 206 kwa  wananchi wa Halmashauri hiyo huku ikitoa wito kwa wananchi na wawekezaji Nchini kuchangamkia Viwanja hivyo.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw George Mkindo wakati akizungumza na Waandishi wa habari Ofisini kwake kuhusiana na uendelezaji wa Halmashauri hiyo.

Anabainisha kuwa Viwanja vilivyopimwa ni  vya Makazi,Hoteli,Kumbi za Starehe,Shule na Maeneo ya  Wazi na kubainisha awali wananchi walivichangamkia Viwanja hivyo lakini kwa sasa mwitikio ni mdogo  wa wananchi kuvinunua.

‘Tulikusudia kupima Viwanja 1000 lakini tumepima Viwanja 700 na tayari viwanja 206 vimeuzwa kwa wananchi na vimebaki  Viwanja 494 hivyo ni wakati wa wananchi  na wawekezaji kuvichangamkia viwanja hivyo’anasema Mkurugenzi huyo.

Akizungumzia uendelezaji wa Halmashauri hiyo anasema kuwa wanakamilisha Ujenzi wa Jengo jipya la Halmashauri ya Mji huo katika maeneo ya Lunyanyu na kwamba wanahimiza ufanyaji  wa kazi kwa juhudi na maarifa kwa wananchi wa Halmashauri hiyo.

No comments:

Post a Comment