Sunday, January 6, 2013

JKT MLALE WATAKIWA KUDUMISHA AMANI,UPENDO NA MSHIKAMANO 2013

Wasema 2012 walitimiza majukumu yao,2013 wataongeza ari ya kutimiza majukumu yao
 Mkuu wa Kikosi cha 842 JKT  Mlale akisalimiana na baadhi ya Askari katika Sherehe za kuuga Mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 zilizofanyika Kikosini hapo hivi karibuni.
 Akishusha kitambaa kama ishara ya kuukaribisha mwaka 2013.Kushoto ni Mkuu wa Utawala wa Kikosi hicho Kapteni Gerald Lwenyagira.
Na Joseph Mwambije
Songea
WANAJESHI katika Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa cha 842 Mlale Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma wametakiwa kuzingatia na kutii miiko ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) ili kudumisha amani na mshikamano uliopo  Nchini.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni wakati wa Sherehe za kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 na Mkuu wa Kikosi hicho Meja Thomas Mpuku wakati akizungumza kwenye sherehe hizo zilizofanyika kikosini hapo.
Alichukua fursa hiyo kuzipongeza familia za Wanajeshi zilizodumisha amani na upendo katika familia zao  kikosini hapo kwa mwaka 2012 na kuzitaka  familia za wanajeshi zilizoshindwa kuishi hivyo zijirekebishe na kuishi kwa amani na upendo mwaka 2013.
Kwa upande wake Mkuu wa utawala wa Kikosi hicho Kapteni Gerald Lwenyagira alisema kuwa kikosi hicho kilijitahidi na kutimiza majukumu yake mwaka 2012 katika malezi ya Vijana,uzalishaji mali na kufanya Operesheni mbalimbali za Kijeshi ikiwemo Operesheni ya miaka 50 ya uhuru na Opersheni Sensa na kwamba kwa mwaka 2013 wataongeza ari ya kutimza majukumu yao.
 Akishusha Kitambaa.
 Akisalimiana na baadhi ya Askari.

Mkuu huyo wa Kikosi Meja Thomas Mpuku akizungumza Kikosini hapo hivi karibuni.Kushoto ni Mkuu wa  Utawala Kikosini hapo Kapteni Gerald Lwenyagira.

No comments:

Post a Comment