Sunday, January 6, 2013

WAHAMASISHWA KUJIUNGA NA NHIF NA MFUKO WA AFYA YA JAMII SONGEA

 Meneja wa Wanachama wa Bima ya Afya Nchini,Ellentruda Mbilinyi akigawa Mashuka kwa Mganga wa Kituo cha Afya Madaba Songea Vijijini,Maxensius Kayombo kwa ajili ya Kituo hicho ambayo kwa pamoja na tisheti yana thamani ya shilingi milioni moja.Katikati anayeshuhudia ni Mratibu wa NHIF Songea,Suzane Mkondya.

 Meneja huyo(katikati) akizungumza na Wanachama wa Bima ya Afya katika Kijiji cha Wino.Kushoto ni Mratibu wa NHIF Mkoa wa Ruvuma,Suzane Mkondya na kulia ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Wino,Notiwele Mtewele.

Msimamizi wa NHIF Mkoa wa Ruvuma,Silively Mgonza akizwahamasisha Wananchi wa Kijiji cha Madaba kujiunga na mfuko huo.
Na Joseph Mwambije,
Songea
WANANCHI Mkoani Ruvuma wamehamasishwa kujiunga na mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na ule wa afya ya Jamii ili waweze kupata huduma za afya zinazokidhi viwango kwa kuwa wanachama wanapo kuwa wengi ndivyo utoaji wa huduma hizo unakuwa rahisi.
Wananchi walihamasishwa kujiunga na huduma hizo juzi katika Kijiji cha Wino Songea Vijijjini Mkoani Ruvuma na Viongozi wa Bima ya afya (NHIF) Kitaifa na Kimkoa ambapo mbali na uhamasishaji huo Viongozi hao pia walitoa mashuka kwa Kituo cha Afya cha Madaba,Zahanati ya Mahanje na ya Wino na tisheti vyote kwa pamoja vikiwa na thamani ya shilingi milioni moja.
Akizungumza kwenye Mkutano uliofanyika katika Zahanati ya Wino uliowahusisha Wananchi wa kijiji Cha Wino na Viongozi wa ngazi ya Kata  na Kijiji hicho pamoja na wanachama wa mfuko huo Meneja wa Wanachama wa Bima ya Afya,Elentruda Mbogoro amewataka Wanachi kujiunga kwa wingi katika mfuko huo uli kurahisisha utoaji wa huduma badala ya kulalamikia huduma zinazotolewa.
Meneja huyo anasema kuwa baadhi ya maeneo huduma za mfuko huo  zinakuwa hazikidhi viwango kwa kuwa wanachama ni wachache hivyo na fedha nazo zinakuwa hazijitoshelezi na kubainisha kuwa dhana ya kusema nachangi huduma lakini siugui si  sahihi.  
‘Unapokuwa umechangia huduma na haujaugua nalo ni jambo jema kwa kuwa hakuna mtu anayependa kuuugua hivyo unakuwa umemchangia mtu mwingine anayeumwa kupata huduma za matibabu’alisema Meneja huyo.
Awali katika Taarifa yake Afisa Mtendaji wa Kata ya Wino,Notiwele Mtewele alisema kuwa Kata hiyo yenye Wakazi 12800 na Vijiji vitano ina wanachama 84 wa huduma ya afya na inakabiliwa na upungufu wa madawa kwenye Zahanati yake.
Naye Msimamizi wa NHIF Mkoa wa Ruvuma,Silively Mgonza anasema kuwa wamejipanga kuondokana na tatizo la dawa kwa kutoa  huduma ya Bima ya afya kwa Maduka ya dawa muhimu yaliyosajiliwa na TFDA na kwamba tayari maduka mawili ya dawa mkoani humo yameanza kutoa huduma hiyo lengo likiwa wananchi wapate huduma ya dawa.
Kwa upande wake Mganga  wa Kituo cha Afya Madaba,Maxencius Mahundi  ameshukuru kwa msaada huo na kubainisha kuwa walikuwa wakikabiliwa na upungufu wa mashuka na kwamba yaliyopo yalikuwa yamechakaa.

 
 Wananchi wa Kata ya Wino Songea wakiwasikiliza Viongozi wa NHIF hivi karibuni.
Mganga wa Kituo cha Afya Madaba  Songea,Maxensius Kayombo akizungumza kwenye Mkutano huo.

No comments:

Post a Comment