Tuesday, January 15, 2013

KUPINGA GESI KUSAFIRISHWA NI KUPINGANA NA BABA WA TAIFA-NCHIMBI


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana(UVCCM) Mkoa wa Ruvuma,Alex Nchimbi akizungumza wakati akifungua Baraza la UVCCM  Mkoa wa Ruvuma.Kulia ni Katibu wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Ruvuma,Mwajuma Rashid.


KUPINGA GESI KUSAFIRISHWA NI KUPINGANA NA BABA WA TAIFA-NCHIMBI

Na Joseph Mwambije
Songea

MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa CCM(UVCCM) Mkoa wa Ruvuma Bw. Alex Nchimbi  amesema kuwa kupinga gesi kusafirishwa kwenda Daressalaam ni kupingana na Baba  wa Taifa Hayati Julius Nyerere  aliyetaka kuwepo na mgawanyo sawa kwa rasilimali za Taifa kwa Mikoa yote Nchini.
Alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua  Barazaza la Vijana wa Chama hicho lililofanyika hivi karibuni mjini Songea na kuwataka Vijana wa Chama hicho kuwa makini wanapozijibia hoja za Kitaifa si kukurupuka kama hiyo ya gesi.
Alisema kuwa Baba wa Taifa  aliweka mgawanyo sawa wa rasilimali za Taifa na kuondoa ubaguzi wa kidini na Kikabila huku akiitambulisha lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya Taifa.
‘Tukisema rasilimali zinufaishe Mkoa husika pekee je Mikoa isiyokuwa na kitu itafanyaje,kwa sisi Mkoa wa Ruvuma mahindi yetu yamekuwa yakilisha Tanzania yote na Nchi nyingine za jirani’alisema.
Aliwataka Vijana hao kushirikiana na Jamii klatika masula ya kijamii pamoja nma elimu katika Shule za Sekondari na Shule za Msingi ambako alidai kuwa huko Umoja huo umekuwa ukipwaya wakati Vyama vya upinzani vimejikita kwa kiwango kikubwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Bw. Joseph Mkirikiti ambaye alikuwepo kwenye Baraza hilo  aliwataka Vijana kushirikiana katika kuijenga Jumuiya yao ya UVCCM na Chama chao kwa ujumla huku wakiwaunga mkono wanaokijenga Chama hicho badala ya kuwapinga.
Alimpongeza mjumbe wa Baraza kuu la Umoja wa Vijana Taifa Bw. Alfan Kigwenembe kwa kazi nzuri ya kufanya mikutano na kuongea na vijana mbalimbali wa Chama hicho na ambao si wa Chama hicho huku akiyazungumzia masuala mbalimbali ya msingi na kuyatolea ufafanuzi.

No comments:

Post a Comment