Tuesday, January 15, 2013

VIJANA MSISUKUMWE KATIKA MAKUNDI YA KUVURUGA AMANI-KIGWENEMBE

 Mjumbe wa Baraza kuu la V ijana wa CCM  Taifa  akizungumza kwa hisia kali katika moja ya mikutano yake.
 Alfan Kigwenembe akizungumza na Vijana katika moja ya Mkikutano yake.
 
VIJANA MSISUKUMWE KATIKA MAKUNDI YA KUVURUGA AMANI-KIGWENEMBE
Na Joseph Mwambije,
Songea
VIJANA  wametakiwa kutosukumwa katika makundi ya kuvuruga amani,kutumika kisiasa na kuandamana bila sababu za msingi na matokeo yake wao ndio wanaoathirika katika vurugu za kisiasa na maandamano na kuziacha familia zao zikiahangaika.
Wito huo ulitolewa juzi na mjumbe wa Baraza kuu la vijana wa CCM(UVCCM)Alfan Kigwenembe  wakati akizungumza na vijana kwenye mkutano wa hadhara katika Kata ya Msamala mjini Songea mambo mbalimbali yanayowahusu Vijana.
Mwanasiasa huyo kijana alikuwa akizungumza na Vijana wote wa Manispaa ya Songea bila kujali itikadi zao za kisiasa kwa kuwa wao ndio rasilimali  ya Taifa na wamekuwa wakitumika vibaya na Wanasiasa kwa maslahi yao.
Alibainisha kuwa katika maandamano zinapotokea fujo vijana wanaathirika kwa kupata ulemavu wa maisha na wakati mwingine kupoteza maisha na kuziacha familia zao zikihangaika huku Viongozi wa  Siasa waliowasukuma kuandamana wakishindwa kuwasaidia na kusaidia familia zao baada ya wao kupoteza maisha.
‘Vijana lazima mtambue kuwa nyinyi ni rasilimali ya Taifa hivyo hampawi kushiriki katika fujo na kuvuruga amani ya Nchi yetu na kuandamana katika maandamano yasiyokuwa ya msingi na badala yake mjiunge katika Vikundi vya ujasiriamali ili mjiletee maendeleo’alisema Mwanasiasa huyo.
Aliwataka vijana kufanya kazi kwa bidii ili kujileteaaendeleo kwa kuwa maisha bora hayaletwi kwa kucheza bao na Pool na badala yake yanaletwa kwa kufanya kazi kwa bidii na kuongeza kuwa miradi mbalimbali ya madini Mkoani Ruvuma ukiwemo wa Urenium utaongeza ajira kwa Vijana.


Alfan Kigwenembe

No comments:

Post a Comment