Wednesday, January 9, 2013

NAIBU WAZIRI WA MAJI AIKATAA TAARIFA YA MKURUGENZI WAMAMLAKA YA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA SONGEA


 SAM_1185.JPG


Mkurugenzi wa maji safi na usafi wa mazingira(SOUWASA) Songea,Mhandisi Francis Kapongo akitoa malezo kwa Naibu Waziri wa maji Mhandisi Binilith Mahenge(kushoto) kuhusu Bwawa la kienyeji la kuhifadhi maji la Ruhila kwenye chanzo cha mto Ruhila.Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi wa SOUWASA,Wilson Mandia.

NAIBU WAZIRI WA MAJI AIKATAA TAARIFA YA MKURUGENZI WA SOUWASA SONGEA
Na Joseph Mwambije
Songea
NAIBU   Waziri wa maji Mhandisi Binilithi Mahenge ameikataa taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji  wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira(SOUWASA) Mhandisi Francis Kapongo kutokana na mapungufu na kutoeleza mapato na matumizi ya fedha inazozipata na zinazotolewa na Serikali na Wafadhili mbalimbali.

Aliikataa taarifa hiyo juzi mara baada ya kusomewa katika ukumbi wa Mamlaka hiyo na kushangazwa kuwa na mapungufu mengi na kutoeleza tatizo la maji lililojitokeza mwaka jana na kupelekea Wizara hiyo kutuma Watalaamu kuja kuchunguza.

‘Hii taarifa ina mapungufu mengi,haina mapato na matumizi na haijaeleza tatizo kubwa la maji lililojitokeza mwaka jana na Wizara ya maji ilivyolishughulikia hivyo basi niandalie taarifa nyingine ili matatizo niweze kuyashughulikia’alisema Naibu Waziri huyo ambeye yuko katika Ziara ya siku tano Mkoani Ruvuma.

Alisema kuwa taarifa hiyo ina mapungufu mengi na haijaeleza wananchi wanahitaji kiasi gani cha maji,mapungufu ni kiasi gani na inatoa huduma kwa wananchi wangapi na kushangazwa na  Mkurugenzi huyo kutoa taarifa yenye mapungufu kiasi hicho na kusema taatifa aliyoitoa haifanani na Nafasi yake.

Naibu Waziri huyo alimtaka Mkurugenzi huyo kumuandalia taarifa nyingine ambayo itaeleza matumizi ya shilingi  bilioni 36 zilizotolewa na Wafadhili kwa kushirikiana na Serikali jinsi zilivyotumika katika Mradi mkubwa wa maji wa mtandao wa maji taka ambao bado haujakamilika.

Alimuagiza Mkurugenzi huyo kuhakikisha Watumiaji wote wa maji ya Mamlaka hiyo wanafungiwa mita na kuwasimamia vizuri Wateja wao katika kulipia maji wanayotumia na wahakikishe Mamlaka hiyo inajiendesha kwa faida na kubainisha kuwa makusanyo ya Mamlaka hiyo ni kidogo.

Awali akisoma taarifa hiyo kwa Naibu Waziri alisema kuwa kuna vyanzo 9 vya chemichemi vilivyopo katika milima ya Matogoro ambavyo huzalisha maji kwa matumizi ya mji wa Songea na kwamba havitoshelezi mahitaji na hivyo chanzo cha mto Luhira hutumika kuongeza wingi wa maji.

Mhandisi Kapongo katika taarifa yake alisema Mtandao wa bomba wa maji safi una urefu kilomita 37 na kwamba mabwawa 6 yamejengwa kwa ajili ya shughuli za kutibu majitaka na kwamba kwa sasa Wateja waliounganishwa na huduma hiyo ni 1020 huku lengo likiwa kuwaunganishia wateja 1500 ifikapo juni 2013.

Alisema kuwa wanajipanga kuongeza vyanzo vipya vya maji na kumalizia ujenzi wa mtandao wa maji safi katika maeneo   katika Kata sita za Manispaa hiyo ambao utagharimu shilingi bilioni 49.52 hadi kukamilika.

Pia alisema kuwa wanajipanga kupanua huduma ya maji taka na maji safi katika maeneo ya mapya ya mji ambayo ni Mshangano,Msamala,Ruhuwiko,Chabruma,Seedfarm,Mateka,Ruvuma kwa shilingi  bilioni 40.314.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Bw. Joseph Mkirikiti alisema atasimamia maagizo yote ya ya Naibu Waziri huyo kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora ya maji na kutatua kero ya maji kwa wananchi.
Mwisho
  SAM_1185.JPGMkurugenzi wa maji safi na usafi wa mazingira(SOUWASA) Songea,Mhandisi Francis Kapongo akitoa malezo kwa Naibu Waziri wa maji Mhandisi Binilith Mahenge(kushoto) kuhusu Bwawa la kienyeji la kuhifadhi maji la Ruhila kwenye chanzo cha mto Ruhila.Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi wa SOUWASA,Wilson Mandia.
SAM_1189.JPG
   Naibu Waziri wa maji Mhandisi  Binilith Mahenge akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Songea Bw. Joseph Mkirikiti(kushoto) na Naibu Meya(kulia) wa Manispaa ya Songea Bw. Willon Kapinga wakati akikagua vyanzo vya maji juzi.
SAM_1191.JPGNaibu Waziri  maji ,Binilith Mahenge akipita kwenye Bwawa la kuhifadhia maji la Matogoro juzi wakati wa Ziara yake ya siku tano ya kukagua miradi ya maji.Kushoto ni Mkurugenzi wa maji safi na usafi wa mazingira(SOUWASA) Songea,Francis Kapongo na kulia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Songea,Willon Kapinga.
  







No comments:

Post a Comment