Friday, January 11, 2013

KAMPUNI NYINGINE TATU ZAIDI NAMTUMBO ZINAFANYA UTAFITI WA MADINI YA URANI

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo-Abdula Lutavi.

Madini ya  Urani yanayotarajiwa kuanza kuchimbwa  Wilayani Namtumbo na Kampuni ya Mantra  Tanzania.
KAMPUNI NYINGINE TATU  ZAIDI  NAMTUMBO ZINAFANYA UTAFITI WA MADINI  YA
 URANI
Na Joseph  Mwambije,
Namtumbo
KAMPUNI tatu zaidi  Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma zinafanya utafiti wa   madini ya Urani  ukiondoa Kampuni ya Mantra Tanzania Limited ambayo iko mbioni kuanza kuchimba madini hayo  na ikiwa madini hayo yataanza kuchimbwa yatainua uchumi wa Wilaya hiyo.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo  Bw. Abdula Lutavi wakati akizungumza na Waandishi wa habari Wilayani humo kuhusu maendeleo ya Wilaya hiyo kwa kipindi cha miaka  saba kuanzia mwaka 2005 hadi 2012.
Mkuu huyo wa Wilaya amezitaja Kampuni hizo kuwa ni Western Metal (T) Ltd,Uranex Tanzania Limited na Frontier Resources Tanzania Limited  na kwamba kupitia Kampuni ya Mantra Tanzania Limited Wilaya hiyo inatarajia kuwa na uwekezaji mkubwa wa madini hayo baada ya makubaliano ya Serikali na Kampuni hiyo kukamilika.
Anasema kuwa kwa kipindi cha miaka saba Wilaya hiyo imepiga hatua kubwa katika masuala mbalimbali ambapo uwezo wa Wilaya hiyo kukusanya mapato kupitia vyanzo vyake vya ndani umeongezeka na kufanya Wilaya hiyo kuweza kuboresha maisha ya Wananchi wake.
‘Tumepiga hatua kubwa katika matumizi  bora ya ardhi ambapo ndani ya kipindi cha miaka saba tumepima Viwanja 7,307,mashamba 52,881.79,vijiji 57,tumetoa hati miliki za mashamba za kimila 6345,hatimiliki za kimila kwa wanawake 835,vyeti vya ardhi za vijiji 38 na tumetenga maeneo 27 kwa ajili ya matumizi bora ya ardhi ’alisema.
Alisema kuwa kwa kipindi cha miaka saba Wilaya hiyo imefanikiwa  kuboresha miundombinu yake ya barabara na  baraba ya lami inayoiunganisha Wilaya hiyo na Wilaya ya Songea inatarajiwa kukamilika  hivi karibuni na kwamba  katika Sekta ya elimu wamefanikiwa kupunguza mimba kwa wanufunzi na wameweka mikakati kuzuia kabisa mimba kwa Wanafunzi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Bw. Mohamed Maje anasema kuwa wameweka mikakati kuipaisha Wilaya hiyo kiuchumi kupitia miradi  mbalimbali ya maendeleo na kupunguza umaskini kwa wananchi wake.
Mwisho


 Mjiolojia wa kampuni  inayotafiti madini ya Urani Namtumbo,John Mtukula akitoa maelezo ya madini hayo wakati Wanahabari hao walipotembelea kwenye eneo la utafiti wa madini hayo Wilayani Namtumbo
 Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo,Mohamed Mataje(kulia) akinong'onezana jambo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Steve Nana.
 Madini ya Urani
 Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari wakizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo.Kutoka kulia Albano Midelo wa gazeti la Kiongozi,Amon Mtega -Mtanzania,Cresensia Kapinga-Majira na Leticia Nyoni Meneja wa Kampuni ya Business Times Ruvuma.
Wanahabari hao wakiwajibika

No comments:

Post a Comment