Saturday, January 12, 2013

WANANCHI WAONYWA KUJENGA KWENYE KINGO ZA MTO

 Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga akimkabidhi Mwenyekiti wa Jumuia ya watumia maji wa Bonde la JUWAMALU Christian Matembo cheti cha usajili wa Jumuia hiyo , mbali na cheti pia alikabidhi fedha taslim na vifaa vya ofisini kwa ajili ya kuanzisha jumuia hiyo .(picha na Joyce Joliga,Mbinga)

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga akimkabidhi Mwenyekiti wa Jumuia ya watumia maji wa Bonde la JUWAMALU Christian Matembo cheti baskeri nne zenye jumla ya thamani ya shilingi 660,000 kwenye ukumbi wa Hoteli ya Mbicu wilayani hapo.(picha na Joyce Joliga,Mbinga)
WAKAZI wa Bonde la Mto Luwaita wilayani mbinga wameonywa  kuacha vetendo vya  kufyatua matofari na kujenga nyumba kwenye kingo za mito ili kuzuia uharibifu wa mazingira na uchafuzi wa maji kwani wakikamatwa wanafanya vitendo hivyo watachukuliwa hatua za kisheria .
Onyo hilo  limetolewa jana kwenye ukumbi wa Hoteli ya Mbicu na Afisa  maji bonde  la   ziwa Nyasa toka makao makuu Tukuyu Witga Nkondora    wakati wa uzinduzi wa Jumuia ya watumia maji wa bonde la JUWAMARU  wilayani Mbinga.
Amesema,bado kuna changamoto mbali mbali ambazo zinawakabili katika utunzaji wa bonde hilo ambapo kuna baadhi ya wananchi wamepimiwa viwanja katika kingo za mito ,kitu ambacho kinarudisha nyuma malengo ya huifadhi wa  bonde hilo.
Ameongeza kuwa,mbali na wananchi kupimiwa viwanja maeneo ya kingo za mito pia wapo ambao wanafanya shuguli za kufyatua matofali, kulima ndani ya vyanzo vya maji hivyo  kuharibu mazingira.
"Tumejipanga kuhakikisha watu wote ambao wanafanya uharibifu kwenye vyanzo vya maji wanachukuliwa hatua za sheria ilikuweza kudhibiti tatizo la uharibufu wa mazingira katika mabonde ,"alisema Nkondola
Awali akizindua Umoja wa watumia maji ,  Mkuu wa wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga amewatataka wakazi wa bonde hilo kulitunza bonde hilo ,na kufanya kazi ya kudhibiti uharibifu wa mazingira kwa uadilifu na uhaminifu mkubwa .
Natambua kazi iliyopo ,mbele yetu ni kubwa na ngumu ,bado wilaya yetu inakabiliwa na changamoto kubwa sana ya uharibifu wa mazingira ,naomba tufanye kazi hii kwa umakini, uzalendo na kwa uadilifu mkubwa iwapo tatutunza vyanzo hivyo vizuri raslimali hiyo itakuwa endelevu,  "alisema Ngaga
Aidha ,ameongeza kuwa serikali ipo pamoja na wananchi na itaendelea kushirikiana nao ili kuhakikisha malengo ya uhifadhi wa mabonde ya maji na vyanzo vya maji yanatunzwa na kulindwa kwa manufaa ya jamii nzima na vizazi vijavyo.

No comments:

Post a Comment