Friday, July 20, 2012

WAWILI WASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMUUA KIKATILI MTOTO WAO MCHANGA KWA KUMNYONGA

WAWILI WASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMUUA KIKATILI MTOTO WAO MCHANGA KWA KUMNYONGA




Na Joseph Mwambije,
Songea

WATU wawili mtu na mkewe katika  Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumuua kinyama kwa kumpiga kwa mawe mtoto wao mchanga wa Miezi saba na kumuweka kwenye Chemba ya Mtaro wa maji  kwa kile kinachodaiwa kuwa ni  Masuala ya kimapenzi.

Ofisa Mtendaji wa Mtaa wa Chemchem  katika Kata ya Matogoro Mkoani humo Bw. Fama Suta amewataja wanaoshikiliwa kuwa ni Bw.  Shangwe  Komba(28) na Mkewe Bi.  Mwazani Chimgege(25) wakazi wa Chemchem Matogoro Mkoani humo.

Amewaambia Waandishi wa habari kuwa tukio hilo lilitokea Julai 16 mwaka huu katika  Mtaa wake ambapo anasema yeye baada ya kufahamishwa kuhusiana na tukio hilo alitoa taarifa Kituo cha Polisi cha Mjini kati kwa njia ya simu.

Kiongozi huyo wa Mtaa  akisimulia jinsi tukio lilivyosikitisha alisema kuwa kwa jinsi tukio lenyewe alivyoliona awali mtoto huyo wa kiume  alinyweshwa sumu  na kunyongwa na kisha kupigwa mawe akiwa kwenye Mtaro wa Chemba ya kupitishia maji. .

‘Mtoto huyo aliuawa  baada ya  kupita wiki moja ya kufanyiwa tohara na kwa kweli ni tukio linalosikitisha ambapo mimi linanifanya niweweseke usiku na katika Mtaa wangu hili ni tukio la kwanza’alisema na kuongeza

Anasema awali Polisi walimkamata Zawadi Komba  dada wa  Mtuhumiwa Shangwe Komba na kumuhoji kuhusiana na tukio hilo ambapo alieleza kuwa  mdogo wake huyo alimuomba ampe sh. 50,000 akamtibu mwanae huyo wa kufikia aliyemuua.

Alisema baada ya kumpa pesa hiyo akaja na kuomba pesa nyingine ambapo akasema hana ampeleke kwa pesa hiyo na endapo atalazwa atakuja Hospitali na baada ya kuelezwa hivyo ndipo akamwambia kuwa amemuua Mwanae anaomba ampe pes nyingine ili akimbie.

Hata hivyo baada ya kumuhoji Mwanamke huyo na kufanikiwa kuwakamata Watuhumiwa kwa ushirikiano wake Polisi  walimuachia huru.

‘Kwa kweli inaonyesha kuwa Mwanaume huyo alishauriana  na Mkewe wamuue mtoto huyo ili waweze kufurahia maisha yao na kutafuta mtoto mwingine kwa kuwa mtoto yule hakuwa wa Mwanaume huyo’alisema.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Deudediti Nsemeki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kubainisha kuwa uchunguzi   wa tukio hilo bado unaendelea ili kubaini  chanzo chake  na kuwafikisha Mahakamani Watumiwa.




No comments:

Post a Comment