Wednesday, August 22, 2012

MWANASHERIA WA CCM AJITOSA KUGOMBEA UNEC KUPITIA WILAYA YA SONGEA VIJIJINI

 Mwanasheria wa CCM Bw. Glorious Luoga akipokea fomu za kugombea ujumbe wa Halmashauri kuu Taifa(NEC)katika Chama cha Mapinduzi toka kwa Katibu wa CCM Songea Vijijini  Bi. Lyidia Gunda.
 Akishukuru toka kwa Katibu huyo baada ya kupokea fomu hizo.
 Akitoa maelezo kwa Katibu.

 Akiwa ametoa fedha za kuchangia Chama hicho na fza fomu.
 Akihesabu fedha za kuchangia Chama hicho kabla hajazitoa.
 Akitoa fedha aa kuchangia Chama kiasi cha shilingi laki moja.
 Aliondoka baada ya zoezi hilo.Mwanasheria huyo amebainiasha kuwa Chama hicho kupitia kwenye misukosuko ndio kuimarika kwake.
 Akizungumza baada ya zoezi la kupokea fomu na kuchangia Chama na kusema anaomba kutumwa kwenda anakokujua ili akivushe Chama hicho katika kipindi hiki kigumu.Kulia ni mama yake mzazi aliyemsindikiza kwenda kuchukua fomu Bi. Antonia Mselewa Diwani wa Viti maalumu Kata ya Madaba.
 Akiendelea kujinasibu kwamba amekuja kuwapokea mkongojo wazee ili kuyaendeleza yale waliyoyaanzisha na kubainisha kuwa tayari amekwishakisaidia chama kutimiza wajibu wake akiwa Mwanasheria wa chama hicho kwa kushinda kesi zote alizozisimamia.
Waandishi wa Vyombo mbalimbali vya habari wakikava Story ya Mwanasheria huyo kuchukua fomu.

No comments:

Post a Comment