Tuesday, September 11, 2012

MATAIFA YA NJE YANATAKA KUTUPIGANISHA NA MALAWI-WAZEE

 Wazee wa Mkoa wa Ruvuma wakimsikiliza Waziri wa mambo ya nje Bw. Benard Membe.
 Wakimpigia makofi wakati akiingia
 Mkuu wa Wilaya ya Songea Bw. Joseph Mkilikiti(katikati) wakati wa kumsubiri Waziri huyo.
 Waziri huyo akizungumza kwenye mkutano huo kuhusu mgogoro wa Mpaka kati ya Tanzania na Malawi na kubainisha kuwa jitihada za usulushishi zimeshindwa hivyo huenda suala hilo likapelekwa kwenye Mahakama za Kimataifa kuamuliwa na kwamba Sheria za Kimataifa zinataka  Nchi zinazoleta Shauri kupeleka suala kwa wadau kabla ya kupelekwa huko na ndicho Tanzania inachokifanya sasa.
 Meme akiwazee hao.
 Membe akisoma ramani ya Ziwa Nyasa inayoonyesha kuwa Mpaka uko katikato ya Ziwa ambayo alipewa na Mzee Emanuel Chilokota mabaye alieleza kwa kina jinsi anavyoifahamu MBAMBA BAY.
 Bado akipitia  ramani hiyo
 Mzee Ally Jaibu akisisitiza kuwa Mpaka uko kati kati ya Ziwa na kwamba Mataifa ya Ulaya yanataka kuzigombanisha Nchi hizi mbili Tanzania na Malawi.
 Mzee Mustapha Njozi(85) ambaye alipigana Vita vya  pili vya dunia anasema kuwa aliwahi kuwauliza Waingereza wakati wa Vita vya pili ya dunia kwamba je itaweza kupiganwa vita nyingine kubwa ndani ya Afrika kama hiyo,wakamjibu kuwa haitapiganwa kwa Matakwa ya Afrika bali Nchi hizo za Ulaya zitaanzisha vita kutaka kuuza na kujaribu  silaha zao huku akisisisitiza kuwa mpaka uko kati kati ya Ziwa bali lengo kubwa ni hilo la Nchi hizo kugombanisha Nchi hizo mbili
 Naye Mzee Chilokota akisisitiza kuwa Mpaka uko kati kati ya ZIWA.
Membe akizungumza.kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu

No comments:

Post a Comment