Thursday, September 13, 2012

Waziri mkuu wa zamani Misri afungwa jela


 Na Mashirika ya habari
Libya
Bw. Nazif Ahmed

 Na Mashirika ya habari
Libya
Bwana Nazif, ambaye alikuwa waziri mkuu kuanzia mwaka 2004 hadi mwaka jana wakati mapinduzi ya kiraia yalipofanyika, pia ameamrishwa kulipa faini ya dola milioni 1.5.
Mwaka jana Ahmed Nazif alifutwa kazi kwa muda wa mwaka mmoja baada ya kushtakiwa kwa kosa la kupata faida haramu kutokana na biashara alizofanya kinyume na sheria.
Nazif alikuwa mmoja wa maafisa wakuu katika serikali ya rais wa zamani Hosni Mubarak.
Alikamatwa miezi kadhaa baada ya kuacha kazi mwezi Januari mwaka 2011, muda mfupi kabla ya rais Mubarak kuachia ngazi.
Maafisa kadhaa wa uliokuwa utawala wa Mubarak wamefikishwa mahakamani kwa aidha kosa la njama ya kuwaua waandamanaji au makosa ya kuhusiana na ufisadi.
Mubarak alihukumiwa kifungo cha maisha jela mwezi Juni baada ya kuhusishwa na mauaji ya waandamanaji.
CHANZO-BBC

No comments:

Post a Comment